Shughuli itakuwa pale kwa Mkapa leo ikizikutanisha Yanga sc na Namungo kwenye mtanange wa NBC Premier League. Jana watani wa Yanga sc, Simba sc waliwalaza Singida Big Stars kwa 3-1 na mashabiki wao walifurahi sana. Leo ni zamu ya Wananchi kupata burudani huku wakitarajia kubaki kileleni kama ilivyo kawaida yao. Je Namungo watafungwa kirahisi? Wananchi mtafurahi leo? Tupe maoni yako kwenye comments.
SPIKA WA BUNGE LA JMT JOB NDUGAI AJIUZULU Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo leo Januari 06, 2022 ikiwa ni siku chache tangu kusambaa kwa video ambayo alinukuliwa akisema ipo siku Nchi itauzwa kutokana na madeni Amesema ameandika Barua ya kujiuzulu kwa Katibu Mkuu wa CCM na uamuzi huo ni binafsi na hiari, na ameuchukua kwa kuzingatia maslahi mapana ya Nchi, Serikali na Chama.