Skip to main content

Posts

Yanga Sc v Namungo Leo

Shughuli itakuwa pale kwa Mkapa leo ikizikutanisha Yanga sc na Namungo kwenye mtanange wa NBC Premier League.  Jana watani wa Yanga sc, Simba sc waliwalaza Singida Big Stars kwa 3-1 na mashabiki wao walifurahi sana. Leo ni zamu ya Wananchi kupata burudani huku wakitarajia kubaki kileleni kama ilivyo kawaida yao. Je Namungo watafungwa kirahisi? Wananchi mtafurahi leo?  Tupe maoni yako kwenye comments. 
Recent posts

Spika Job Ndugai Abwaga Manyanga

SPIKA WA BUNGE LA JMT JOB NDUGAI AJIUZULU Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo leo Januari 06, 2022 ikiwa ni siku chache tangu kusambaa kwa video ambayo alinukuliwa akisema ipo siku Nchi itauzwa kutokana na madeni Amesema ameandika Barua ya kujiuzulu kwa Katibu Mkuu wa CCM na uamuzi huo ni binafsi na hiari, na ameuchukua kwa kuzingatia maslahi mapana ya Nchi, Serikali na Chama.

Simba na Yanga Zagawa Dozi Mapinduzi Cup

Katika michezo iliyopigwa jana ya Mapinduzi Cup wababe wa soka Tanzania Simba na Yanga waligawa dozi muruwa na kuleta furaha na burudani kwa mashabiki wao. Simba wakicheza mchezo wao majira ya saa 10 jioni waliwabamiza Selem View fc kwa 2-0 huku magoli yao yakifungwa na Sakho pamoja na Bwalya.  Yanga wakikipiga milango ya saa 2 na robo usiku wakawafurumusha timu ya Taifa Jang'ombe kwa 2-0 huku magoli yao yakipigwa na Heritier Makambo (mzee wa kuwajaza) pamoja na Denis Nkane the wonder Kid aliyesajiliwa akitokea Biashara United.  Timu zote za Kariakoo Dar es Salaam zilicheza zikiwakosa nyota wao kadhaa ambao huwa wanaanza kwenye kikosi cha kwanza lakini bado zilisalia zikiwa mwiba vile vile. Je wewe umeonaje viwango vya Simba na Yanga bila baadhi ya nyota wao? Basi usiache ku comment ili tupate mawazo yako.

RAIS MAGUFULI: UGONJWA USIWE SABABU YA KURUDI NYUMA.

RAIS MAGUFULI: KAMWE UGONJWA HUU USIWE SABABU YA KURUDI NYUMA “Ndugu Wafanyakazi wenzangu nawapongeza sana kwa kuchapa kazi, mimi nipo pamoja nanyi na natambua kazi nzuri mnayoifanya, nawaomba katika kipindi hiki ambacho dunia inapita katika wakati mgumu wa kukabiliana na ugonjwa wa #Corona, sisi tuendelee kuchapakazi, kamwe ugonjwa huu usiwe sababu ya kurudi nyuma na kuacha kuwahudumia Watanzania, mimi naamini Mwenyezi Mungu atatuvusha, ” - Rais Magufuli. #RaisMagufuli amewapongeza na kuwatakia heri wafanyakazi wote hapa nchini ambao leo tarehe 01 Mei, 2020 wanaadhimisha siku ya wafanyakazi #MeiMosi. Mwaka huu sherehe za Mei Mosi hazitafanyika ili kuepusha mikusanyiko ya watu, ikiwa ni hatua muhimu ya kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa homa ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona (Covid-19). # MwenyeziMunguAtuvusha #Covid19 #CoronaTanzania #CoronaDeaths #VifoCorona Credit: #AZAMTV

Rais Dk. John P. Magufuli atangaza kifo cha Balozi Dk. augustine Mahiga

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.John Pombe Magufuli anatangaza kifo cha Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Balozi Dkt Augustine Philip Mahiga (Mbunge) kilichotokea leo Alfajiri tarehe 01 Mei, 2020.. Mhe.Balozi Mahiga ameugua ghafla akiwa nyumbani kwake. #ITVTanzania

WAGONJWA 37 WAPONA CORONA, 71 WASUBIRI VIPIMO VYA MWISHO

WAGONJWA 37 WAPONA CORONA, 71 WASUBIRI VIPIMO VYA MWISHO Wagonjwa 37 waliokuwa wameambukizwa virusi vya Corona #COVID19 wamepona na kuruhusiwa kurejea nyumbani baada ya vipimo vya mwisho kuthibitisha kwamba hawana maambukizi. “Watu hawa 108 hawana dalili zozote za ugonjwa kama vile homa au mwili kuchoka isipokuwa wapo katika vituo vya matibabu kusubiri vipimo vya mwisho ili kuthibika kwamba hawana virusi vya corona kabla ya kuruhusiwa kutoka vituoni,” amesema Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu. Waziri Ummy Mwalimu amewataka watu waliopona ugonjwa huo kuzingatia maelekezo ya wataalamu wa afya ili kujikinga na maambukizi mapya ya COVID-19 kwani zipo tafiti zilizofanyika nchi mbalimbali ikiwamo China zimeonyesha kuwa watu wanaweza kupata maambukizi mapya kama asilimia 14. “Tunapenda kuwahimiza watu waliopona watoe elimu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona (COVID-19) kwa jamii. Pia, Nitumie fursa hii kwa niaba ya Serikali kutoa shukrani

*GSM WAFANYA SURPRISE KWA WACHEZAJI WA YANGA*

*GSM WAFANYA SUPRISE KWA WACHEZAJI WA YANGA* Mdhamini wa Klabu ya Yanga leo alifanya Suprise ambayo wachezaji hawakuwa wameitarajia. Wachezaji wa Yanga waliitwa na Meneja wa Timu Abeid Mziba kuwa anaomba kukutana nao Mlimani City Bila kuwaambia anakusudia kufanya nini kwa wachezaji hao. Baada ya wachezaji kufika Mlimani City walipelekwa moja kwa moja kwenye Duka la GSM ndani ya Mlimani City na kukabidhiwa VOCHA YA SH. LAKI SITA KILA mchezaji na kutakiwa kutumia VOCHA hiyo kwenye maduka Ya GSM kwa kujipatia Bidhaa wanayoitaka. Wachezaji walifurahishwa sana na Jambo hilo. Nasasa GSM inakusudia kuwaalika wachezaji Waliooa kuwapeleka Wake zao kwa Suprise ambayo GSM hakuitanabahisha. Wachezaji ambao wapo nje ya Dar watakutana na Vocha zao wakirejea. Tazama picha Mbali mbali wakati wachezaji wa Yanga walipokuwa wakijipatia Mahitaji yao ndani ya Duka la GSM Mlimani City Leo 20/04/2020. @bigbros_tanzania_tv