Skip to main content

WANAFUNZI WAUA IRINGA

Wanafunzi wa Chuo cha Uuguzi cha Bulongwa kilichoko Wilaya ya Makete mkoani Iringa, wamemuua kwa kumshambulia kichwani mkufunzi wa chuo hicho, Dk. Jumbe Mafingo, kwa madai ya kupinga jaribio lake la kutaka kumbaka mwanafunzi mwenzao.

Taarifa za awali za makachero wa polisi zilieleza kuwa mkufunzi huyo aliuawa baada ya kutuhumiwa kwamba alitaka kumdhalilisha kijinsia mwanafunzi wa kike, Jean Laison Mwakabuta kwa kutaka kumbaka.
Tukio hilo la kuuawa kinyama kwa mkufunzi huyo ambaye ni mwalimu wa nidhamu chuoni hapo, lilitokea juzi usiku nyumbani kwake mjini hapa.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Evarist Mangalla, Dk. Mafingo alifikwa na umauti baada ya mwanafunzi huyo kuamua kwenda nyumbani kwake usiku ili kumkabidhi maelezo yake ya kimaandishi kuhusu sababu zilizomfanya alale nje ya chuo.

Ilielezwa kuwa muda mfupi baada ya kuingia kwenye nyumba ya mwalimu huyo, mwanafunzi huyo alianza kupiga kelele kuwa anabakwa.

Kamanda wa Polisi Mkoani Iringa Bwana Evarist Mangalla

Alisema kufuatia kelele hizo, wanachuo wengine waliamka katika vyumba vyao na kwenda hadi eneo la tukio na kuanza kumshambulia kichwani mkufunzi huyo hadi kumuua.

Kamanda Mangalla alisema Dk. Mafingo aliuawa kwa kushambuliwa na kitu kizito kichwani.

“Huyu Jean Laison Mwakabuta, aliambiwa na Dk. Mafingo ambaye ni mwalimu wa nidhamu chuoni hapo, aandike maelezo ya maandishi kwa sababu gani alilala nje ya chuo,...baada ya kuandika maelezo hayo, aliamua kuyapeleka nyumbani kwa mkufunzi huyo usiku, sasa baada ya kugonga mlango na hatimaye akaruhusiwa kuingia, alianza kupiga kelele kwamba anabakwa…na ndipo wanafunzi wenzake waliposikia kelele wakaamka na kukimbilia eneo hilo na kumshambulia mkufunzi huyo hadi kufa,” alisema Kamanda Mangalla.

Ilidaiwa kuwa siku moja kabla ya tukio hilo, uongozi wa chuo hicho cha Bulongwa ulitoa ridhaa kwa wanachuo wote kwenda kutembea nje ya chuo kwa lengo la kuwapunguzia msongo wa mawazo ya masomo na Jean Laison Mwakabuta hakurejea chuoni hadi siku iliyofuata.

Kamanda Mangalla, alisema wanachuo wanne akiwamo mwanafunzi Jean, wametiwa mbaroni kuhusiana na mauaji hayo.

Chanzo: Nipashe

Comments

Popular posts from this blog

These are Said to Be the Best Goalkeepers in the World, Ranking from 1-25

25. Stephane Ruffier, Saint-Etienne Had Stephane Ruffier not sustained a groin injury in 2011, Monaco might never have been relegated to Ligue 2. But he did, and they were, and that summer the then-24-year-old goalkeeper joined Saint-Etienne, rebuffing Manchester City in the progress. This season he played all 38 Ligue 1 matches for Les Verts for a second season in succession, conceding just 32 goals as his side finished a surprising fifth in the standings and qualified for the Europa League. 24. Pepe Reina, Liverpool Only Joe Hart kept more Premier League clean sheets than Pepe Reina in 2012-13. In a season that saw Liverpool finish a disappointing seventh in the English top-flight, the 30-year-old managed to keep things respectable from a defensive standpoint, conceding only 34 goals and stopping 88 per cent of the shots he faced. To finish the season he conceded just a single goal in his last four matches. 23. Mariano Andujar, Catania Only Parma managed ...

The Happy Di Matteo..!

Roberto Di Matteo watched his attacking stars inspire a 5-4 extra-time victory over Manchester United and he preferred to savour a second night of high-scoring league cup thrills rather than focus on "the other stuff" in football. The Chelsea manager did not need to spell out what he meant, in the wake of the league fixture against United on Sunday, when his team's controversial 3-2 home defeat was followed by the allegation that the referee Mark Clattenburg had racially abused Mikel John Obi. There had also been spite in the stands. Di Matteo focused on the flair and spirit that his team had shown here, when they came from behind three times to force the extra period, with the substitute Eden Hazard scoring from the penalty spot with the very last kick of normal time. Hazard's quick feet and sumptuous reverse pass created what proved to be the decisive fifth goal late in extra-time for Ramires. "Over the last two days we have seen...

Read What Shakira Says. Via Yahoo!

Looking at  Shakira  and her fabulous figure you might be surprised to learn it was only three months ago that she gave birth to son Milan. But the “Hips Don’t Lie” singer reveals that dropping the pounds was no cake walk. While promoting “The Voice” in Pasadena, California, on Monday, the blond bombshell revealed, "[Losing baby weight] is the only thing that’s been a little stressful … I knew I had to come back here to do ‘The Voice’ two months after I had delivered a baby. I didn’t have my four months of maternity like every woman on Earth has. I’m not trying to complain, but it’s been a process full of challenges.” Photo source: omg INSIDER & Yahoo The 36-year-old mama added that the pressure to shed the baby weight at record speed is something that she feels the previous generations didn't face. She said, “I think that our mothers and grandmothers weren’t under the pressure women of today are after delivering a baby. My dad says there’s nothing better than meat...