Skip to main content

Habari Zaidi Kuhusu Chelsea Hizi Hapa

1. Fernando Torres Awaasa Wenzake

 Fernando Torres ambaye inaonekana ameuanza msimu vizuri sana

Amewaambai wenzake kwamba kama wanataka kuutwaa ubingwa wa Uingereza basi wasifanye makosa yoyote katika msimu huu wa ligi.

Kesho Jumamosi 25 Julai Chelsea watapambana na Newcastle kwenye uwanja wa Stamford Bridge wakiwa kileleni mwa ligi kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2010 baada ya kushinda mechi zao mbili za kwanza.

Torres alisema, "Hatuwezi kupoteza mechi mapema kwani Man City walishinda mechi nyingi msimu uliopita. Hivyo tunahitaji kuanza ligi vizuri. Siku zote ni muhimu kuanza vizuri na ukiangalia msimamo unaiona Chelsea iko juu. Pointi tisa kwa mechi tatu za kwanza ndilo lengo letu." Alisema Muhispania huyo wa Chelsea na kuongeza, "Ni muhimu baada ya mechi 10 kwa timu kuendelea kubakia kileleni, hivyo itamaanisha kwamba hiyo ndiyo nafasi yako."

Msimu uliopita Chelsea walishinda ligi ya mabingwa pamoja na FA Cup lakini Torres anakubali kwamba kushika nafasi ya sita kwenye kwenye ligi inaonesha ni jinsi gani wanahitaji kuongeza juhudi.

Torres aliongeza kusema, "Premier League inaonesha uko kwenye levo gani kwa sababu inachezwa kwa mwaka mzima, lakini mashindano ya kugombea Kombe fulani ni tofauti. Sisi ni timu kubwa na nzuri, tuna uwezo na mbinu nyingi za kupambana na kushinda vikombe na tunaweza kuifunga timu yoyote lakini ligi inakuonesha levo uliyopo na msimu uliopita tulimaliza nafasi ya sita. Ni lazima tuongeze juhudi." Aliendelea kusema, "Ni lazima tutambue kuwa ligi ya mabingwa siyo rahisi kushinda kila mwaka hivyo hatua ya kwanza ni kuwa kwenye nne bora-hicho ni kitu cha kawaida kwa Chelsea. Sasa lazima tuutafute ubingwa wa Uingereza, kama unawaza nafasi ya kwanza basi unaweza kuifikia, hata ya pili na ya tatu, lakini kama unawaza tu kuwa ndani ya nne bora basi unaweza kupoteza."

Torres akiwa katika moja wapo ya wakati wake wa shangwe

Torres aliianza kampeni yake vizuri hasa baada ya kufunga dhidi ya Man City kwenye Community Shield na mechi kati yao na Reading ambapo walishinda 4-2.

Ivanovic alisema, "Didier Drogba alikuwa ni wa muda mrefu sana, na ni mmoja kati ya wachezaji muhimu wa timu hii. Kuwakosa wachezaji kama yeye ni ngumu sana. Kila mtu anajua jinsi gani atacheza na hakuna anayeweza kumzuia. Sasa tumebadilika sana, siyo washambuliaji tu bali safu yote ya mbele. Kila mmoja anafuraha na kumwamini Fernando. Anafanya kazi nzuri sana. Anafanya mengi sana kwa timu na tunafurahi sana kumwona akifunga kwa sababu anastahili. Tunafahamu jinsi gani atacheza msimu huu."


2. Cesar Azpilicueta Akamalisha Saini Yake Chelsea


Mlinzi huyu wa Uhispania amekamilisha uhamisho wake toka Marseille kwenda Chelsea. Mchezaji huyo mwenye miaka 22 ambaye ni beki wa kulia imeripotiwa kwamba amejiunga na mabingwa hao wa Ulaya kwa dola milioni 7.

Azpilicueta ambaye ameiwakilisha Spain kwenye mashindano mbalimbali ya vijana na alishiriki mashinda ya Olympic yaliyoisha siku chache zilizopita, alisafiri kwenda Uingereza usiku wa jana ili kutia saini yake Chelsea na hivyo alikosa mechi ya timu yake ya Europa League qualifier dhidi ya FC Sheriff Tiraspol iliyopigwa jana usiku.

"Timu ya Chelsea inayofuraha kutangaza kwamba Cesar Azpilicueta  amesaini kuichezea timu yetu." Ilisema taarifa toka Uongozi wa Chelsea.

3. Ofa Ya Chelsea Kumchukua Moses Yakubalika

 
 Huyu ni Victor Moses wa Wigan Athletic

Timu ya Wigan imekubali ofa toka kwa Chelsea ya kutaka kumsajili mchezaji wao Victor Moses.

Chombo kimoja cha habari kilisema jana usiku kwamba baada ya Wigan kukubali ofa ya Chelsea wamempa ruhusa Moses afanye mazungumzo na timu ya Chelsea.

Habari toka Wigan zilisema, "Timu  yetu inathibitisha kwamba baada ya maombi manne toka Chelsea ya kumtaka Moses kugonga mwamba, ombi lao la tano leo limefanikiwa baada ya kukutana na matakwa na masharti yetu. Hivyo mchezaji amepewa ruhusa ya kuzungumza na Chelsea."


Comments

Popular posts from this blog

These are Said to Be the Best Goalkeepers in the World, Ranking from 1-25

25. Stephane Ruffier, Saint-Etienne Had Stephane Ruffier not sustained a groin injury in 2011, Monaco might never have been relegated to Ligue 2. But he did, and they were, and that summer the then-24-year-old goalkeeper joined Saint-Etienne, rebuffing Manchester City in the progress. This season he played all 38 Ligue 1 matches for Les Verts for a second season in succession, conceding just 32 goals as his side finished a surprising fifth in the standings and qualified for the Europa League. 24. Pepe Reina, Liverpool Only Joe Hart kept more Premier League clean sheets than Pepe Reina in 2012-13. In a season that saw Liverpool finish a disappointing seventh in the English top-flight, the 30-year-old managed to keep things respectable from a defensive standpoint, conceding only 34 goals and stopping 88 per cent of the shots he faced. To finish the season he conceded just a single goal in his last four matches. 23. Mariano Andujar, Catania Only Parma managed ...

The Happy Di Matteo..!

Roberto Di Matteo watched his attacking stars inspire a 5-4 extra-time victory over Manchester United and he preferred to savour a second night of high-scoring league cup thrills rather than focus on "the other stuff" in football. The Chelsea manager did not need to spell out what he meant, in the wake of the league fixture against United on Sunday, when his team's controversial 3-2 home defeat was followed by the allegation that the referee Mark Clattenburg had racially abused Mikel John Obi. There had also been spite in the stands. Di Matteo focused on the flair and spirit that his team had shown here, when they came from behind three times to force the extra period, with the substitute Eden Hazard scoring from the penalty spot with the very last kick of normal time. Hazard's quick feet and sumptuous reverse pass created what proved to be the decisive fifth goal late in extra-time for Ramires. "Over the last two days we have seen...

Read What Shakira Says. Via Yahoo!

Looking at  Shakira  and her fabulous figure you might be surprised to learn it was only three months ago that she gave birth to son Milan. But the “Hips Don’t Lie” singer reveals that dropping the pounds was no cake walk. While promoting “The Voice” in Pasadena, California, on Monday, the blond bombshell revealed, "[Losing baby weight] is the only thing that’s been a little stressful … I knew I had to come back here to do ‘The Voice’ two months after I had delivered a baby. I didn’t have my four months of maternity like every woman on Earth has. I’m not trying to complain, but it’s been a process full of challenges.” Photo source: omg INSIDER & Yahoo The 36-year-old mama added that the pressure to shed the baby weight at record speed is something that she feels the previous generations didn't face. She said, “I think that our mothers and grandmothers weren’t under the pressure women of today are after delivering a baby. My dad says there’s nothing better than meat...