Skip to main content

Unamfahamu Antonio Valencia? Huyu Hapa

 Valencia akiwa kwenye moja ya harakati zake za kuchonga krosi

Alijiunga na Manchester United mwaka 2009 kwa donge la dola milioni 17. Naye ni raia wa Ecuador.  Ilikuwa ni wakati Christiano Ronaldo anahamia Real Madrid na kuacha pengo kubwa sana kwa Man United. Pengo ambalo hakuna aliyewahi kuwaza kwamba lingezibika.

Lakini mara alipoanza kuichezea Man United alianza kuonesha kwamba anaweza kwani mbio pamoja na krosi zake kuelekea upande pinzani vilikuwa ni hatari tupu.

 Alianza vizuri sana lakini akakumbwa na balaa la kuumia kiasi kwamba alikaa nje ya dimba kwa muda na kufanya watu washindwe kushuhudia uwezo wake vizuri.

Msimu uliopita ndipo watu walipoona umuhimu wake na kipaji chake na kugundua kwamba ni winga wa kiwango cha juu sana. Akiwa na uwezo wa kukimbia na mpira kwenye wing ya kulia na kuachia mashuti yake  ya krosi kama risasi zikiwa zinawalenga Wayne Rooney pamoja na Javier Hernandez.

Winga huyo ambaye watu hudhani ni old fashion, hapendi sana kupiga chenga badala yake ni kukimbia na kutoa krosi, alifunga magoli 6 na kusababisha 13, huku ni David Silva pekee akiwa juu yake kwa kusababisha magoli 15 kwenye mechi nyingi.

Msimu ambao alifanya juhudi sana bila kuchoka na mashabiki wa Man United wakamzawadia "Mchezaji bora wa mwaka" na zawadi ya goli la msimu kwa goli alilofunga walipocheza dhidi ya Blackburn Rovers.

Udhaifu pekee ambao mashabiki wa Man United wanauona kwake ni kule kushindwa kwake kutumia mguu wa kushoto wakati wa mchezo. Japo alijaribu kupiga krosi kwa mguu wa kushoto pale walipopambana na Fulham.

Ni mchezaji ambaye kwa kweli anastahili kuwa hapo alipo leo. Valencia, mwenye miaka 27 sasa, ana uwezo bado wa kukuza soka lake na kuwa moja ya wachezaji wa kukumbukwa duniani. Hakuna maswali mengi sana juu ya hilo kwani sasa anavaa namba ya jezi iliyovaliwa na wachezi maarufu sana duniani.

Wewe unasemaje kuhusu Valencia?

Comments

Popular posts from this blog

These are Said to Be the Best Goalkeepers in the World, Ranking from 1-25

25. Stephane Ruffier, Saint-Etienne Had Stephane Ruffier not sustained a groin injury in 2011, Monaco might never have been relegated to Ligue 2. But he did, and they were, and that summer the then-24-year-old goalkeeper joined Saint-Etienne, rebuffing Manchester City in the progress. This season he played all 38 Ligue 1 matches for Les Verts for a second season in succession, conceding just 32 goals as his side finished a surprising fifth in the standings and qualified for the Europa League. 24. Pepe Reina, Liverpool Only Joe Hart kept more Premier League clean sheets than Pepe Reina in 2012-13. In a season that saw Liverpool finish a disappointing seventh in the English top-flight, the 30-year-old managed to keep things respectable from a defensive standpoint, conceding only 34 goals and stopping 88 per cent of the shots he faced. To finish the season he conceded just a single goal in his last four matches. 23. Mariano Andujar, Catania Only Parma managed ...

Hawa Ndiyo Real Madrid Waliowafunga Man City Champions League Jana Usiku

Man City wakiwa wanaongo za kwa 2-1 dhidi ya Real Madrid huku zikiwa zimebaki dakika si zaidi  ya tatu walionekana kama ingekuwa ni timu ya tatu ya Uingereza kuifunga Madrid kwenye uwanja wa Bernabeu. Lakini vijana hao wa Mancini badala ya kuinza kampeni yao kwa ushindi walijikuta wakiachwa nyuma na kuwaangalia Madrid wakiibuka na ushindi baada ya Karim Benzema kusawazisha na kisha Cristiano Ronaldo kufunga goli la tatu na la ushindi, goli lililomfanya bosi wao Jose Mourinho kuslide uwanjani akishangilia goli hilo na Ronaldo. This was the real happiness now from Ronaldo BBC football pundit Robbie Savage alikuwa uwanjani huku Bernabeu. (quoting from BBC SPORTS) "Maicon was not at the races at all in the first half at right-back. He was a passenger and it was like City were playing with 10 men. Cristiano Ronaldo kept coming inside him. "In the second-half, Vincent Kompany looked at what was happening and came across to that wing more. Ronaldo did not...

MANCHESTER UNITED VS CHELSEA #EPL TODAY AT OLD TRAFFORD STADIUM

MANCHESTER UNITED vs CHELSEA FC LEO #EPL USIKOSE NA USIKUBALI KUSIMULIWA #TheBattleAtOldTrafford:  Jioni ya leo miamba ya kabumbu la Uingereza inakutana katika mpambano unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua. Manchester United leo wanawakaribisha mahasimu wao Chelsea pale Old Trafford kwenye mchezo wa round ya pili ya Premier League. Ikumbukwe kuwa Katika mchezo wa kwanza walipokutana pale Stamford Bridge Chelsea waliwanyuka Man United 1-0,  goli lililofungwa na Alvaro Morata kwa kichwa. Kuna kama kauadui flani hivi kati ya makocha Antonio Conte wa Chelsea na José Mourinho wa Man United. Na huu ni uhasimu ambao kila mmoja wao anajaribu kuuficha na kuonesha kuwa hawana shida kati yao. Mourinho amenena kuwa game kati ya timu hizi mbili ni ya kawaida kwake kama game nyingine nyingine na hakuna chochote special kuihusu. Lukaku, Rashford, Martial,  Matic,  Pogba, De Gea  na wengineo wanategemewa kuongoza kikosi cha man United leo huku Morata, Fabregas, Pe...