Skip to main content

Spurs Yawachapa Kipigo Red Devils

Clint Dempsey jana aliwathibitishia ushindi Tottenham kwa mara ya kwanza wakiwa Old Trafford tangu  December 1989 baada ya kuwapa kipigo mashetani hao wekundu (Man United) na kuwafanya kupoteza mchezo wa pili tangu kuanza kwa ligi hiyo ya Uingereza. 

Huyu ndiye Clint Dempsey akishangilia goli

Wakiwa wanaongoza 2-0 hadi half-time, Spurs walikianza kipindi cha pili kwa kuruhusu goli toka kwa Man United lililofungwa na Luis Nani aliyepokea krosi toka kwa Wayne Rooney ambao waliingia kipindi cha pili kama simba aliyejeruhiwa, lakini muda mfupi tu baada ya kuruhusu goli hilo walipiga tena goli la tatu na kuwafanya vijana wa Man United wachanganyikiwe. Lakini Man United walijitahidi kucheza bila kuonesha kama wamechanganyikiwa na kuelekeza mashambulizi makali langoni mwa Spurs huku wakicheza kandanda safi lililowafanya Spurs kupaki gari kuanzia katikati ya uwanja hadi ndani ya eneo lao la 18, huku Rafael, Wayne Rooney, Evra na hata Rio Ferdinand wakipeleka krosi za kila mara langoni mwa wapinzani wao wakijaribi kutafuta kusawazisha na hata kupata goli la ushindi. Lakini alikuwa ni Shinji Kagawa aliyewapatia Man United goli la pili na la mwisho na kuufanya mchezo kwisha kwa Spurs kuibuka kwa ushindi wa 3-2.

Spurs wakiwa bado hawajapoteza mchezo tangu kufunguliwa kwa ligi hiyo, wanajipatia umaarufu na kujiamini sana chini ya kocha wao Andre Villas-Boas, aliyekuwa kocha wa zamani wa Porto. 

Kuumia kwa Nemanja Vidic kulileta pengo kubwa sana kwa upande wa Man United na kusababisha katikati kuwe na kichochoro ambacho kiliwapatia Spurs urahisi wa kufunga magoli  yao. Pamoja na wachezaji wakongwe Ryan Giggs na Paul Scholes, bado kullikuwa na udhaifu mkubwa kwani Spurs walionekana wenye mbio na nguvu wakiwa na maumbo makubwa zaidi ya Man United. 

Giggs na  Scholes wanashindwa siku hizi kuonesha ule umaarufu wao wa kutawala kiungo na ile tabia ya Giggs kupiga krosi zinazowarahisishia wafungaji kupata magoli mazuri. Kwani walionekana kuzidiwa sana na wachezaji wenye kasi na nguvu nyika Gareth Bale na Moussa Dembele, na kufanya kuonekana kama vile chaguo la Ferguson ni ajali iliyokuwa inasubiriwa kutokea. 

Pamoja na kwamba hakukuwa na wa kumlaumu kati yao kwa goli la Vertonghen kwenye dakika ya 2 tu ya mchezo, lakini ilioneka wazi aliachiwa nafasi ya wazi ya kukimbia kuanzia katikati ya dimba kabla ya kufunga goli. 

Vertonghen, aliyetokea Ajax, aliwapita Nani na Rio Ferdinand wakati alipokimbia kwa mita 35 na shuti lake kumgonga beki wa Man United John Evans kabla halitinga wavuni.

Chelsea wameendelea kubakia kileleni baada ya Juan Mata kuifanya iibuke kwa ushindi wa 2-1 ugenini dhidi ya Arsenal. Wapo pointi 3 mbele ya Everon ambao nao waliendelea na ushindi wa 3-1 dhidi ya Southampton. 

Mabingwa watetezi wa Premier League Manchester City wakitokea nyuma walishinda 2-1 dhidi  ya Fulham, wakimuingiza Edin Dzeko aliyewapatia goli la ushindi dakika 3 kabla ya mtanange kuisha.

 

Comments

What an enjoyable time to look through to this post thanks for the sharing and keep it up.
RKAY said…
Thank you very much. It means a lot to me. I sure will keep it up. Join in me almost everyday.

Popular posts from this blog

These are Said to Be the Best Goalkeepers in the World, Ranking from 1-25

25. Stephane Ruffier, Saint-Etienne Had Stephane Ruffier not sustained a groin injury in 2011, Monaco might never have been relegated to Ligue 2. But he did, and they were, and that summer the then-24-year-old goalkeeper joined Saint-Etienne, rebuffing Manchester City in the progress. This season he played all 38 Ligue 1 matches for Les Verts for a second season in succession, conceding just 32 goals as his side finished a surprising fifth in the standings and qualified for the Europa League. 24. Pepe Reina, Liverpool Only Joe Hart kept more Premier League clean sheets than Pepe Reina in 2012-13. In a season that saw Liverpool finish a disappointing seventh in the English top-flight, the 30-year-old managed to keep things respectable from a defensive standpoint, conceding only 34 goals and stopping 88 per cent of the shots he faced. To finish the season he conceded just a single goal in his last four matches. 23. Mariano Andujar, Catania Only Parma managed ...

MANCHESTER UNITED VS CHELSEA #EPL TODAY AT OLD TRAFFORD STADIUM

MANCHESTER UNITED vs CHELSEA FC LEO #EPL USIKOSE NA USIKUBALI KUSIMULIWA #TheBattleAtOldTrafford:  Jioni ya leo miamba ya kabumbu la Uingereza inakutana katika mpambano unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua. Manchester United leo wanawakaribisha mahasimu wao Chelsea pale Old Trafford kwenye mchezo wa round ya pili ya Premier League. Ikumbukwe kuwa Katika mchezo wa kwanza walipokutana pale Stamford Bridge Chelsea waliwanyuka Man United 1-0,  goli lililofungwa na Alvaro Morata kwa kichwa. Kuna kama kauadui flani hivi kati ya makocha Antonio Conte wa Chelsea na José Mourinho wa Man United. Na huu ni uhasimu ambao kila mmoja wao anajaribu kuuficha na kuonesha kuwa hawana shida kati yao. Mourinho amenena kuwa game kati ya timu hizi mbili ni ya kawaida kwake kama game nyingine nyingine na hakuna chochote special kuihusu. Lukaku, Rashford, Martial,  Matic,  Pogba, De Gea  na wengineo wanategemewa kuongoza kikosi cha man United leo huku Morata, Fabregas, Pe...

This is How Manchester City Won Easily Against Sunderland

The New York Times Reported that, Manchester City turned on the style Saturday, easing to a 3-0 victory over visiting Sunderland that lifted the team to second place in England’s Premier League Aleksandar Kolarov scored from a free kick after five minutes, and Sergio Agüero and James Milner added goals in the second half to secure a convincing win.  By ending Sunderland’s unbeaten start, City maintained its own and won consecutive league matches for the first time this season.  “We played very well and took no risks,” City Manager Roberto Mancini told Sky Sports television. The team rediscovered its defensive solidity even without its back-line linchpin and captain, Vincent Kompany, who was out with a calf injury.  Micah Richards made a surprise return from an ankle injury, and Joleon Lescott was also restored to the defense. Yaya Touré took over as captain, playing alongside Gareth Barry in the midfield, while Carlos Tévez and Mario...