Skip to main content

Charles James Kahela, Aliyenusurika Kuuawa kwa Bomu Arusha Amefunguka!

MLIPUKO WA BOMU ARUSHA

Charles James Kahela

Bwana Charles James Kahela, mkazi wa Arusha hadi sasa anaona kama ni muujiza kwake kubaki hai,  kwani haamini na wala haelewi kwa nini yeye apone wengine wafe.
Akitoa ushuhuda wake kanisani, Bwana Charles alisema,

"Baada ya kutoka kazini niliamua kupitia kwenye mkutano wa Chadema ambao ndio ulikuwa unafikia mwisho na kwa sababu mahali pale palikuwa karibu sana na kwa bosi wangu, nikaamua ngoja nami nisipitwe niende kusikiliza chochote kutoka kwa mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Bwana Freeman Mbowe." Alifuta machozi, kisha akaendelea. 

"Wakati mkutano umefika mwisho na watu wakiondoa baadhi ya vitu uwanjani huku viongozi nao wakiowa wametoka jukwaani, nilisikia kitu kimerushwa nyuma yangu karibu kabisa na kichwa changu na kwenda kutua mbela ambako kulikuwa bado na watu wengi tu na watoto kadhaa. Nikasikia mlipuko mkubwa sana, baada ya muda nikaona watu wamelala chini na damu nyingi sana zikimwagika. Kweli ilikuwa ni hatari sana, sijawahi kuona tukio baya kama hilo. Muda si muda polisi waliwazingira viongozi wa Chadema kwa ajili ya ulinzi huku wengine wakianza kurusha risasi kuelekea upande wa wananchi waliokuwa wakitoa kipigo kwa mtu mmoja aliyedhaniwa kuonekana akirusha bomu. Ilikuwa ni hatari tupu. Ilinibidi kuvunja mojawapo ya mageti ya mbao ya nyumba jirani na kulala chini ili kukwepa risasi ambazo zilikuwa zilirushwa chini chini sana. Mpaka sasa hivi ninavyoongea bado mwilini  mwangu nasikia joto sana na kutetemeka." Alimaliza Bwana Charles.

Kwa mujibu wa taarifa ya habari ya Redio One Stereo ya saa 2:00 usiku, serikali ilisema kwamba mlipuko uliotokea kwenye mkutano wa Chadema ilikuwa ni bomu la kutupwa kwa mkono. Waziri wa Mambo ya Ndani Dr Emmanuel Nchimbi aliyasema hayo wakati alipowatembelea waathirika wa bomu hilo katika hospitali za Mount Meru, St. Elizabeth na Serani zote za Jijini Arusha.

Nao uongozi wa mkoa wa Arusha umewaomba wananchi kuweka pembeni itikadi zao za kisiasa na kushirikiana kuwabaini watu waliohusika na milipuko wa bomu 

Comments

Popular posts from this blog

These are Said to Be the Best Goalkeepers in the World, Ranking from 1-25

25. Stephane Ruffier, Saint-Etienne Had Stephane Ruffier not sustained a groin injury in 2011, Monaco might never have been relegated to Ligue 2. But he did, and they were, and that summer the then-24-year-old goalkeeper joined Saint-Etienne, rebuffing Manchester City in the progress. This season he played all 38 Ligue 1 matches for Les Verts for a second season in succession, conceding just 32 goals as his side finished a surprising fifth in the standings and qualified for the Europa League. 24. Pepe Reina, Liverpool Only Joe Hart kept more Premier League clean sheets than Pepe Reina in 2012-13. In a season that saw Liverpool finish a disappointing seventh in the English top-flight, the 30-year-old managed to keep things respectable from a defensive standpoint, conceding only 34 goals and stopping 88 per cent of the shots he faced. To finish the season he conceded just a single goal in his last four matches. 23. Mariano Andujar, Catania Only Parma managed ...

Hawa Ndiyo Real Madrid Waliowafunga Man City Champions League Jana Usiku

Man City wakiwa wanaongo za kwa 2-1 dhidi ya Real Madrid huku zikiwa zimebaki dakika si zaidi  ya tatu walionekana kama ingekuwa ni timu ya tatu ya Uingereza kuifunga Madrid kwenye uwanja wa Bernabeu. Lakini vijana hao wa Mancini badala ya kuinza kampeni yao kwa ushindi walijikuta wakiachwa nyuma na kuwaangalia Madrid wakiibuka na ushindi baada ya Karim Benzema kusawazisha na kisha Cristiano Ronaldo kufunga goli la tatu na la ushindi, goli lililomfanya bosi wao Jose Mourinho kuslide uwanjani akishangilia goli hilo na Ronaldo. This was the real happiness now from Ronaldo BBC football pundit Robbie Savage alikuwa uwanjani huku Bernabeu. (quoting from BBC SPORTS) "Maicon was not at the races at all in the first half at right-back. He was a passenger and it was like City were playing with 10 men. Cristiano Ronaldo kept coming inside him. "In the second-half, Vincent Kompany looked at what was happening and came across to that wing more. Ronaldo did not...

MANCHESTER UNITED VS CHELSEA #EPL TODAY AT OLD TRAFFORD STADIUM

MANCHESTER UNITED vs CHELSEA FC LEO #EPL USIKOSE NA USIKUBALI KUSIMULIWA #TheBattleAtOldTrafford:  Jioni ya leo miamba ya kabumbu la Uingereza inakutana katika mpambano unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua. Manchester United leo wanawakaribisha mahasimu wao Chelsea pale Old Trafford kwenye mchezo wa round ya pili ya Premier League. Ikumbukwe kuwa Katika mchezo wa kwanza walipokutana pale Stamford Bridge Chelsea waliwanyuka Man United 1-0,  goli lililofungwa na Alvaro Morata kwa kichwa. Kuna kama kauadui flani hivi kati ya makocha Antonio Conte wa Chelsea na José Mourinho wa Man United. Na huu ni uhasimu ambao kila mmoja wao anajaribu kuuficha na kuonesha kuwa hawana shida kati yao. Mourinho amenena kuwa game kati ya timu hizi mbili ni ya kawaida kwake kama game nyingine nyingine na hakuna chochote special kuihusu. Lukaku, Rashford, Martial,  Matic,  Pogba, De Gea  na wengineo wanategemewa kuongoza kikosi cha man United leo huku Morata, Fabregas, Pe...