Skip to main content

Muendelezo wa Habari Kuhusu Samuel Eto'o

Samuel Eto'o amepania kuwaonesha Chelsea na Jose Mourinho kwamba walikuwa sahihi kusitisha usajili wa Wayne Rooney.  




Mcameroon huyo ameachana na club yake ya Urusi ya  Anzhi Makhachkala na kutia saini kwa mkataba wa mwaka mmoja na kuungana tena na  Mourinho, ambaye alikuwa meneja wake walipokuwa Inter Milan.

Wayne Rooney, baada ya kupewa saa 48 na Mourinho ili atoe uamuzi, 
jibu lake lilikuwa 'No, nabaki United.'

Mourinho amekuwa akifuatilia mchezaji wa Manchester United Rooney, walakini baada ya kukataliwa mara mbili,  Chelsea waliamua kugeukia upande wa pili wa Samuel Eto'o. 

"Nilikuwa na nafasi kadhaa za kuja Uingereza hapo awali, pamoja na ile ya kwanza wakati Mourinho alipokuwa hapa, lakini haikuwezekana kwa sababu moja ama nyingine." Alisema  Eto'o katika mtandao wa chelseafc.com.


"Tangu wakati huo nimekuwa na kazi nzuri na mwenye bahati ya kushinda makombe mengi kwenye nchi tofauti tofauti, lakini moja ya ndoto zangu za mwisho kama mchezaji wa kulipwa ni kuja na kucheza Uingereza na kuona kama nitaweza kupata mafanikio kama niliyoyapata kwenye timu nyingine.  Nina furaha sana kuwepo hapa na natamani nianze kucheza mara moja."  Alieleza Eto'o.

Mchezaji huyo wa zamani wa Barcelona hajasafiri na Chelsea kwenye mchuano wa  European Super Cup dhidi ya  Bayern Munich - yeye wala  Willian, ambaye uhamisho wake toka  Anzhi ulithibitishwa siku ya Jumatano iliyopita.  

Eto'o atapaswa kusubiri hadi  international break ndipo aanze kuonekana uwanjani, watakapokuwa ugenini kupambana na  Everton  September 14. 

Uhamisho wake huo inaonekana usingefanyika endapo Mourinho angekubaliwa kumchukua Rooney.  

Mourinho alisema: "niliwaambia niliyopaswa kusema, nadhani niliweka wazi sana  hatukupeleka ombi la tatu, hatuna zaidi cha kusema, Rooney ni mchezaji wa Man United na hakuna cha ziada."I  

Kumpata  Eto'o, ambaye imelipotiwa kuwa alikuwa akilipwa  £300,000 kwa wiki huko Urusi, ni kinyume na taratibu za Chelsea za kusaini wachezaji vijana. Hali hii pia inaacha swali juu ya mustakabali wa Demba Ba and Fernando Torres kwani Mourinho ameweka wazi kwamba kuwa na washambuliaji wanne ni too much na kufunguka kwa kusema kuwa Romelu Lukaku ndiye tegemeo la badaye kwa Chelsea.  

Nafasi ya Ba kwenye kikosi hicho ipo hatarini, lakini Torres bado anahitaji kulipa  £50million kwa Liverpool, kama Mourihno alivyoweka wazi mapema wiki hii.  


Comments

Popular posts from this blog

These are Said to Be the Best Goalkeepers in the World, Ranking from 1-25

25. Stephane Ruffier, Saint-Etienne Had Stephane Ruffier not sustained a groin injury in 2011, Monaco might never have been relegated to Ligue 2. But he did, and they were, and that summer the then-24-year-old goalkeeper joined Saint-Etienne, rebuffing Manchester City in the progress. This season he played all 38 Ligue 1 matches for Les Verts for a second season in succession, conceding just 32 goals as his side finished a surprising fifth in the standings and qualified for the Europa League. 24. Pepe Reina, Liverpool Only Joe Hart kept more Premier League clean sheets than Pepe Reina in 2012-13. In a season that saw Liverpool finish a disappointing seventh in the English top-flight, the 30-year-old managed to keep things respectable from a defensive standpoint, conceding only 34 goals and stopping 88 per cent of the shots he faced. To finish the season he conceded just a single goal in his last four matches. 23. Mariano Andujar, Catania Only Parma managed ...

MANCHESTER UNITED VS CHELSEA #EPL TODAY AT OLD TRAFFORD STADIUM

MANCHESTER UNITED vs CHELSEA FC LEO #EPL USIKOSE NA USIKUBALI KUSIMULIWA #TheBattleAtOldTrafford:  Jioni ya leo miamba ya kabumbu la Uingereza inakutana katika mpambano unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua. Manchester United leo wanawakaribisha mahasimu wao Chelsea pale Old Trafford kwenye mchezo wa round ya pili ya Premier League. Ikumbukwe kuwa Katika mchezo wa kwanza walipokutana pale Stamford Bridge Chelsea waliwanyuka Man United 1-0,  goli lililofungwa na Alvaro Morata kwa kichwa. Kuna kama kauadui flani hivi kati ya makocha Antonio Conte wa Chelsea na José Mourinho wa Man United. Na huu ni uhasimu ambao kila mmoja wao anajaribu kuuficha na kuonesha kuwa hawana shida kati yao. Mourinho amenena kuwa game kati ya timu hizi mbili ni ya kawaida kwake kama game nyingine nyingine na hakuna chochote special kuihusu. Lukaku, Rashford, Martial,  Matic,  Pogba, De Gea  na wengineo wanategemewa kuongoza kikosi cha man United leo huku Morata, Fabregas, Pe...

FT: TAIFA STARS 2 DRC 0. #SAMATTA NA #KICHUYA

FT:  TAIFA STARS 2, DRC THE LEOPOLDS 0 TAIFA stars leo wamewatoa watanzania kimasomaso baada ya kuwaadabisha The LEOPOLDS DRC kwa kuwaburuza kwa magoli 2-0 katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliopigwa kwenye dimba la Taifa jioni leo. Hadi kipindi cha kwanza kinaisha hakukuwa na timu yoyote iliyoona lango la mwenzake. Lakini kunako kipindi cha pili timu zote mbili zikicheza mpira wa umakini zaidi huku zikiviziana na kushambuliana kwa zamu ilishuhudiwa Mbwana Samatta akiandika bao la kwanza kwa Stars na huku dakika zikiyoyoma Shiza Kichuya akaipatia Stars goli la pili. Naweza kusema leo Stars wamecheza mpira wa kujituma na kujiamini na wenye akili na usikivu toka kwa kocha wao huku Yondani, Nyoni na Gadiel wakiongoza safu ya ulinzi yenye umakini sana; na Samatta,  Kichuya na Simon Msuva wakiisumbua vibaya sana lango la wakongoman. Kabla mechi ya leo,  Stars walipambana na Algeria na kuambulia kipigo cha 4-1 wakiwa ugenini. #Hongera #TaifaStars