Skip to main content

Liverpool 1 vs Man United 0; Arsenal 1 vs Spurs 0. As It Happened at CR PUB in Arusha

Hii ni jana majira ya kuanzia saa tisa hivi alasiri wakati wa mpambano mkali wa kukata na shoka kati ya Liverpool na Manchester United wa Premier League ya kule Uingereza. Ambapo Liverpool waliweza kuutumia uwanja wao wa nyumbani kwa kuwachabanga Man United 1-0. Goli ambalo lilifungwa na Sturidge kunako dakika ya 3 tu ya mchezo huo, na goli hilo kudumu hadi mwisho wa mchezo.

Hapa Arusha kumekuwa na msemo miongoni mwa washabiki wa Liverpool aka "You will never walk alone" kuwa goli linalofungwa na mshambuliaji wao machachari sana aliyesajiliwa msimu uliopita kutokea Chelsea Sturidge hua halisawazishwi na kwamba pindi anapofunga goli tu wana uwezo wa kumtoa golikipa wao ili goli libaki wazi kwani hakuna timu yenye uwezo wa kusawazisha goli lake. Msemo huo sasa ulitimia kwa mashabiki wa Man United ambao walidhani ni mzaha mzaha tu na kwamba wakati wowote timu yao ingesazisha bao hilo. lakini wapi.....! Basi hadi mwisho wa matanange huo Liverpool 1, Man United 0. Hongera kwa Liverpool...! It was a good soccer you showed with good winning spirit...!

Hapa chini nimekuwekea picha za mashabiki wa mechi za jana walipokuwa wakifuatilia mipambano hiyo kwenye club moja inayoonesha Ligi ya Uingereza kpitia DSTV... CR PUB-ARUSHA njia ya kwenda Moshono. 

 mashabiki wa Man United na Liverpool wakifuatilia mpambano 

 mashabiki wa Man United na Liverpool wakifuatilia mpambano 

Huyu ni mshabiki machachari sana wa Arsenal kwa jina ni Erasto Martin na jana alikuwa 
ni mwenye furaha sana baada ya timu yake kuwafunga Spurs 1-0. 

 Huyu ni mshabiki machachari sana wa Arsenal Erasto Martin 
akiwa amekaa na mshabiki wa Man United maarufu kama Munasiju mara baada ya
 United kufungwa na mechi yao kuisha

 Munasiju, shabiki nguli wa Man United akifwatilia mpambano

 Huyu hapa ni shabiki wa Liverpool akiwa amestarehe akiamini 
kwamba goli la Sturidge halirudishwagi.

Huyu ndiyo alikuwa kituko kabisa. Kwanza alikuwa kalewa, 
pili alikuwa anashabikia kwa nguvu zote timu yake ya Arsenal 
na kuwabeza Man United kwamba watakapo kutana nao wajiandae kwa kipigo kikali.

Comments

Popular posts from this blog

These are Said to Be the Best Goalkeepers in the World, Ranking from 1-25

25. Stephane Ruffier, Saint-Etienne Had Stephane Ruffier not sustained a groin injury in 2011, Monaco might never have been relegated to Ligue 2. But he did, and they were, and that summer the then-24-year-old goalkeeper joined Saint-Etienne, rebuffing Manchester City in the progress. This season he played all 38 Ligue 1 matches for Les Verts for a second season in succession, conceding just 32 goals as his side finished a surprising fifth in the standings and qualified for the Europa League. 24. Pepe Reina, Liverpool Only Joe Hart kept more Premier League clean sheets than Pepe Reina in 2012-13. In a season that saw Liverpool finish a disappointing seventh in the English top-flight, the 30-year-old managed to keep things respectable from a defensive standpoint, conceding only 34 goals and stopping 88 per cent of the shots he faced. To finish the season he conceded just a single goal in his last four matches. 23. Mariano Andujar, Catania Only Parma managed ...

Hawa Ndiyo Real Madrid Waliowafunga Man City Champions League Jana Usiku

Man City wakiwa wanaongo za kwa 2-1 dhidi ya Real Madrid huku zikiwa zimebaki dakika si zaidi  ya tatu walionekana kama ingekuwa ni timu ya tatu ya Uingereza kuifunga Madrid kwenye uwanja wa Bernabeu. Lakini vijana hao wa Mancini badala ya kuinza kampeni yao kwa ushindi walijikuta wakiachwa nyuma na kuwaangalia Madrid wakiibuka na ushindi baada ya Karim Benzema kusawazisha na kisha Cristiano Ronaldo kufunga goli la tatu na la ushindi, goli lililomfanya bosi wao Jose Mourinho kuslide uwanjani akishangilia goli hilo na Ronaldo. This was the real happiness now from Ronaldo BBC football pundit Robbie Savage alikuwa uwanjani huku Bernabeu. (quoting from BBC SPORTS) "Maicon was not at the races at all in the first half at right-back. He was a passenger and it was like City were playing with 10 men. Cristiano Ronaldo kept coming inside him. "In the second-half, Vincent Kompany looked at what was happening and came across to that wing more. Ronaldo did not...

MANCHESTER UNITED VS CHELSEA #EPL TODAY AT OLD TRAFFORD STADIUM

MANCHESTER UNITED vs CHELSEA FC LEO #EPL USIKOSE NA USIKUBALI KUSIMULIWA #TheBattleAtOldTrafford:  Jioni ya leo miamba ya kabumbu la Uingereza inakutana katika mpambano unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua. Manchester United leo wanawakaribisha mahasimu wao Chelsea pale Old Trafford kwenye mchezo wa round ya pili ya Premier League. Ikumbukwe kuwa Katika mchezo wa kwanza walipokutana pale Stamford Bridge Chelsea waliwanyuka Man United 1-0,  goli lililofungwa na Alvaro Morata kwa kichwa. Kuna kama kauadui flani hivi kati ya makocha Antonio Conte wa Chelsea na José Mourinho wa Man United. Na huu ni uhasimu ambao kila mmoja wao anajaribu kuuficha na kuonesha kuwa hawana shida kati yao. Mourinho amenena kuwa game kati ya timu hizi mbili ni ya kawaida kwake kama game nyingine nyingine na hakuna chochote special kuihusu. Lukaku, Rashford, Martial,  Matic,  Pogba, De Gea  na wengineo wanategemewa kuongoza kikosi cha man United leo huku Morata, Fabregas, Pe...