Skip to main content

LIGI KUU BARA YAWA SHUBIRI KWA WANA MSIMBAZI

Baada ya kusubiri miezi, wiki, siku na hata saa hadi dakika hatimaye wakati ulitimia pale ulipotokea mtanange mkali wa kukata na shoka kama sio mundu kati ya watani ama maadui wa jadi katika soka la bongo, Yanga na Simba, mchezo uliopigwa kwenye dimba la taifa huku ukitawaliwa na mbwembwe, fitina na majigambo toka kwa mashabiki wa pande zote mbili.

Mchezo ambao tumeshuhudia wana Jangwani Dar Young Africans wakiwazodoa watani wao alimaarufu wekundu wa msimbazi kwa kuwachapa magoli mawili moja katika kila kipindi cha mchezo huo.

Alikuwa ni Donald Ngoma aliyewainia mashabiki wa jangwani kwa kupachika bao baada ya kuunasa mpira uliopigwa na mabeki wa Simba wakirudisha pasi nyumba, ndipo akawalamba chenga beki na kipa wake na kuukwamisha wavuni.

Simba walijaribu kwa nguvu zote kurudi mchezoni na kufanikiwa kushambulia mara kadhaa lakini hadi kipindi cha kwanza kinaisha Yanga 1-0 Simba.

Kipindi cha pili nacho kilianza kwa kasi huku kila timu ikipanga mashambilizi lakini walionekana ni Yanga waliojipanga na ushindi leo baada ya Hamis Tambwe kuwainua wana Jangwani tena na kupachika goli safi sana katika dakika ya 27 kipindi cha pili.

Simba walijaribu kujitutumua ili angalao wapate hata goli la kufutia machozi au kusawazisha lakini siku haikuwa yao leo ukizingatia kwa muda mrefu wamecheza wakiwa pungugu baada ya mmoja wao kupewa kadi nyekundu.

Hivyo hadi mwisho wa mchezo huo uliowaweka kileleni Yanga kwa kufikisha alama 46, Yanga 2, Simba 0.

Comments

Popular posts from this blog

These are Said to Be the Best Goalkeepers in the World, Ranking from 1-25

25. Stephane Ruffier, Saint-Etienne Had Stephane Ruffier not sustained a groin injury in 2011, Monaco might never have been relegated to Ligue 2. But he did, and they were, and that summer the then-24-year-old goalkeeper joined Saint-Etienne, rebuffing Manchester City in the progress. This season he played all 38 Ligue 1 matches for Les Verts for a second season in succession, conceding just 32 goals as his side finished a surprising fifth in the standings and qualified for the Europa League. 24. Pepe Reina, Liverpool Only Joe Hart kept more Premier League clean sheets than Pepe Reina in 2012-13. In a season that saw Liverpool finish a disappointing seventh in the English top-flight, the 30-year-old managed to keep things respectable from a defensive standpoint, conceding only 34 goals and stopping 88 per cent of the shots he faced. To finish the season he conceded just a single goal in his last four matches. 23. Mariano Andujar, Catania Only Parma managed ...

Hawa Ndiyo Real Madrid Waliowafunga Man City Champions League Jana Usiku

Man City wakiwa wanaongo za kwa 2-1 dhidi ya Real Madrid huku zikiwa zimebaki dakika si zaidi  ya tatu walionekana kama ingekuwa ni timu ya tatu ya Uingereza kuifunga Madrid kwenye uwanja wa Bernabeu. Lakini vijana hao wa Mancini badala ya kuinza kampeni yao kwa ushindi walijikuta wakiachwa nyuma na kuwaangalia Madrid wakiibuka na ushindi baada ya Karim Benzema kusawazisha na kisha Cristiano Ronaldo kufunga goli la tatu na la ushindi, goli lililomfanya bosi wao Jose Mourinho kuslide uwanjani akishangilia goli hilo na Ronaldo. This was the real happiness now from Ronaldo BBC football pundit Robbie Savage alikuwa uwanjani huku Bernabeu. (quoting from BBC SPORTS) "Maicon was not at the races at all in the first half at right-back. He was a passenger and it was like City were playing with 10 men. Cristiano Ronaldo kept coming inside him. "In the second-half, Vincent Kompany looked at what was happening and came across to that wing more. Ronaldo did not...

MANCHESTER UNITED VS CHELSEA #EPL TODAY AT OLD TRAFFORD STADIUM

MANCHESTER UNITED vs CHELSEA FC LEO #EPL USIKOSE NA USIKUBALI KUSIMULIWA #TheBattleAtOldTrafford:  Jioni ya leo miamba ya kabumbu la Uingereza inakutana katika mpambano unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua. Manchester United leo wanawakaribisha mahasimu wao Chelsea pale Old Trafford kwenye mchezo wa round ya pili ya Premier League. Ikumbukwe kuwa Katika mchezo wa kwanza walipokutana pale Stamford Bridge Chelsea waliwanyuka Man United 1-0,  goli lililofungwa na Alvaro Morata kwa kichwa. Kuna kama kauadui flani hivi kati ya makocha Antonio Conte wa Chelsea na José Mourinho wa Man United. Na huu ni uhasimu ambao kila mmoja wao anajaribu kuuficha na kuonesha kuwa hawana shida kati yao. Mourinho amenena kuwa game kati ya timu hizi mbili ni ya kawaida kwake kama game nyingine nyingine na hakuna chochote special kuihusu. Lukaku, Rashford, Martial,  Matic,  Pogba, De Gea  na wengineo wanategemewa kuongoza kikosi cha man United leo huku Morata, Fabregas, Pe...