Skip to main content

Tha ''Battle'' Of FA CUP Chelsea vs Man United

Ukiangalia kwa haraka haraka unaweza kutoa matokeo ya mechi hii hata kabla haijachezwa na wala hakuna mtu atakaekushangaa kwa huo ndio mtazamo wa mashabiki wengi wa soka na hata wataalam wa uchambuzi wa kimataifa wa soka. Kwanza Manchester United alichezea kichapo cha magoli 4-0 pale Darajani wakati wa mechi yao ya Premier League dhidi ya Chelsea, mechi ambayo kwa mujibu wa Jose Mourinho ni kwamba 'ilianza na goli' hivyo hakujua nani wa kumlaumu. Leo Man United na Mourihno wanarudi tena Darajani katika robo fainali hii ya FA cup wakiwa na kumbukumbu zile zile za kichapo.

Kwa matazamo mwingine ukiiangalia Manchester United utagundua sio ile iliyopigwa 4=0 na Chelsea kwa maana kwamba imebadilika kwa kiasi kikubwa wakiwa na ari, nguvu na determination ya ushindi, huku wakiwa wamecheza mechi nyingi zaidi bila kupoteza katika mashindano mbalimbali ya ndani na ya nje.

Lakini je, Manchester United wakiwa ndio mabingwa watetezi wa kombe hili la FA watakubali kuupoteza mchezo huu muhimu kwao hata kama wanakutana na Chelsea ambao wanaonekana kuwa na nguvu zaidi yao. Lakini pia je, Chelsea wao wapo tayari kweli kuupoteza mchezo huu na hatimae wayaage mashindano haya kwa kufungwa na Man United? Hayo ni maswali tu ambayo unapaswa kujiuliza na nina uhakika majibu utakayojipatia yatakuchanganya hata wewe mwenyewe kwani mechi hii inatarajiwa kuwa ngumu na inayofananishwa na fainali.

Mourihno, meneja wa Manchester United akidai kuwa kuna uwezekano Chelsea wakacheza mchezo wa kujilinda zaidi kitu ambacho kinapingwa na Konte, meneja wa Chelsea.

Mourinho akimzungumzia Rashford

"Ni maamuzi yake mwenyewe. Anajua kuwa ndiye mshambuliaji pekee mwenye nafasi kubwa ya kucheza na hawezi kukwepa hilo'' 

VIKOSI
CHELSEA
Courtois; Azpilicueta, Luiz, Cahill; Moses, Kante,  Matic, Alonso; Willian, Costa, Hazard.
Substitutes Begovic, Fabregas,  Zouma, Pedro, Batshuayi, Terry, Chalobah. 

MAN UNITED
De Gea; Jones, Smalling, Rojo; Valencia,  Ander Herrera, Pogba, Darmian; Mkhitaryan, Rashford, Young.
Substitutes Romero,  Bailly, Mata, Lingard, Carrick, Blind, Romero, Fellaini.

 Referee Michael Oliver (Northumberland)

Comments

Popular posts from this blog

These are Said to Be the Best Goalkeepers in the World, Ranking from 1-25

25. Stephane Ruffier, Saint-Etienne Had Stephane Ruffier not sustained a groin injury in 2011, Monaco might never have been relegated to Ligue 2. But he did, and they were, and that summer the then-24-year-old goalkeeper joined Saint-Etienne, rebuffing Manchester City in the progress. This season he played all 38 Ligue 1 matches for Les Verts for a second season in succession, conceding just 32 goals as his side finished a surprising fifth in the standings and qualified for the Europa League. 24. Pepe Reina, Liverpool Only Joe Hart kept more Premier League clean sheets than Pepe Reina in 2012-13. In a season that saw Liverpool finish a disappointing seventh in the English top-flight, the 30-year-old managed to keep things respectable from a defensive standpoint, conceding only 34 goals and stopping 88 per cent of the shots he faced. To finish the season he conceded just a single goal in his last four matches. 23. Mariano Andujar, Catania Only Parma managed ...

MANCHESTER UNITED VS CHELSEA #EPL TODAY AT OLD TRAFFORD STADIUM

MANCHESTER UNITED vs CHELSEA FC LEO #EPL USIKOSE NA USIKUBALI KUSIMULIWA #TheBattleAtOldTrafford:  Jioni ya leo miamba ya kabumbu la Uingereza inakutana katika mpambano unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua. Manchester United leo wanawakaribisha mahasimu wao Chelsea pale Old Trafford kwenye mchezo wa round ya pili ya Premier League. Ikumbukwe kuwa Katika mchezo wa kwanza walipokutana pale Stamford Bridge Chelsea waliwanyuka Man United 1-0,  goli lililofungwa na Alvaro Morata kwa kichwa. Kuna kama kauadui flani hivi kati ya makocha Antonio Conte wa Chelsea na José Mourinho wa Man United. Na huu ni uhasimu ambao kila mmoja wao anajaribu kuuficha na kuonesha kuwa hawana shida kati yao. Mourinho amenena kuwa game kati ya timu hizi mbili ni ya kawaida kwake kama game nyingine nyingine na hakuna chochote special kuihusu. Lukaku, Rashford, Martial,  Matic,  Pogba, De Gea  na wengineo wanategemewa kuongoza kikosi cha man United leo huku Morata, Fabregas, Pe...

FT: TAIFA STARS 2 DRC 0. #SAMATTA NA #KICHUYA

FT:  TAIFA STARS 2, DRC THE LEOPOLDS 0 TAIFA stars leo wamewatoa watanzania kimasomaso baada ya kuwaadabisha The LEOPOLDS DRC kwa kuwaburuza kwa magoli 2-0 katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliopigwa kwenye dimba la Taifa jioni leo. Hadi kipindi cha kwanza kinaisha hakukuwa na timu yoyote iliyoona lango la mwenzake. Lakini kunako kipindi cha pili timu zote mbili zikicheza mpira wa umakini zaidi huku zikiviziana na kushambuliana kwa zamu ilishuhudiwa Mbwana Samatta akiandika bao la kwanza kwa Stars na huku dakika zikiyoyoma Shiza Kichuya akaipatia Stars goli la pili. Naweza kusema leo Stars wamecheza mpira wa kujituma na kujiamini na wenye akili na usikivu toka kwa kocha wao huku Yondani, Nyoni na Gadiel wakiongoza safu ya ulinzi yenye umakini sana; na Samatta,  Kichuya na Simon Msuva wakiisumbua vibaya sana lango la wakongoman. Kabla mechi ya leo,  Stars walipambana na Algeria na kuambulia kipigo cha 4-1 wakiwa ugenini. #Hongera #TaifaStars