Skip to main content

MANCHESTER UNITED WALIPA KISASI KWA HUDDERSFIELD. WASHINDA 2-0

Magoli yaliyofungwa na Romelu Lukaku na Alexis Sanchez yalitosha kuizamisha Huddersfield walipowatembelea Manchester United Old Trafford Jana Jumamosi katika mchezo uliochezwa saa 12 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Kichapo hicho walichotoa United ni kama kisasi kwani katika mzunguko wa kwanza walizimwa kwa 2-1 na Huddersfield. Japo mbali na kichapo ushindi huo umekuwa muhimu sana kwao kwani unawahakikishia kubaki nafasi ya pili na kupunguza umbali au utofauti wa alama kati yao na vinara wa ligi msimu huu Manchester City ambapo sasa kuna tofauti ya alama 13 kati yao. 

Lukaku alifungua matumaini ya ushindi jana baada ya kuunganisha krosi safi iliyopigwa na Juan Mata kunako dakika ya 58 kipindi cha pili. Kunako dakika ya 68 Alexis Sanchez aliangushwa ndani ya 18 za Huddersfield na refa kuamuru ipigwe penati. Sanchez alipiga penati hiyo lakini kipa wa Huddersfield aliiona na kuicheza na kwa bahati mbaya kwake na nzuri kwa Sanchez ilimrudia na kuuweka mpira nyavuni na kuandika goli la pili kwa United.

Sanchez alikuwa na mchango mkubwa sana katika ushindi wa United jana hasa kipindi cha pili. Alionekana akicheza kwa nguvu zote,  akitumia akili nyingi  na alijikuta akichezewa madhambi mara nyingi sana kuliko mchezaji yeyote jana. Hata Juan Mata alipata mpira toka kwa Sanchez kabla hajapiga krosi iliyomkuta Lukaku.

Kwenye kipindi cha kwanza ilionekana United walistahili kuzawadiwa penati baada ya McTominay kuchezewa madhambi mabaya sana lakini refa alikataa kutoa penati badala yake ikageuka kuwa fair play.

Juan Mata aliibuka kuwa man of the match kutokana na mchango wake mkubwa kwenye mchezo huo na kwa jinsi alivyokuwa imara sana kwenye eneo la kiungo na kuunganisha wengine kimchezo.

Pogba,  Rashford na Martial waliingia kipindi cha pili baada ya Lukaku, Lingard na Mata kupumzishwa.

Jumapili ijayo Manchester United watawatembela Newcastle United.

Comments

Popular posts from this blog

These are Said to Be the Best Goalkeepers in the World, Ranking from 1-25

25. Stephane Ruffier, Saint-Etienne Had Stephane Ruffier not sustained a groin injury in 2011, Monaco might never have been relegated to Ligue 2. But he did, and they were, and that summer the then-24-year-old goalkeeper joined Saint-Etienne, rebuffing Manchester City in the progress. This season he played all 38 Ligue 1 matches for Les Verts for a second season in succession, conceding just 32 goals as his side finished a surprising fifth in the standings and qualified for the Europa League. 24. Pepe Reina, Liverpool Only Joe Hart kept more Premier League clean sheets than Pepe Reina in 2012-13. In a season that saw Liverpool finish a disappointing seventh in the English top-flight, the 30-year-old managed to keep things respectable from a defensive standpoint, conceding only 34 goals and stopping 88 per cent of the shots he faced. To finish the season he conceded just a single goal in his last four matches. 23. Mariano Andujar, Catania Only Parma managed ...

Hawa Ndiyo Real Madrid Waliowafunga Man City Champions League Jana Usiku

Man City wakiwa wanaongo za kwa 2-1 dhidi ya Real Madrid huku zikiwa zimebaki dakika si zaidi  ya tatu walionekana kama ingekuwa ni timu ya tatu ya Uingereza kuifunga Madrid kwenye uwanja wa Bernabeu. Lakini vijana hao wa Mancini badala ya kuinza kampeni yao kwa ushindi walijikuta wakiachwa nyuma na kuwaangalia Madrid wakiibuka na ushindi baada ya Karim Benzema kusawazisha na kisha Cristiano Ronaldo kufunga goli la tatu na la ushindi, goli lililomfanya bosi wao Jose Mourinho kuslide uwanjani akishangilia goli hilo na Ronaldo. This was the real happiness now from Ronaldo BBC football pundit Robbie Savage alikuwa uwanjani huku Bernabeu. (quoting from BBC SPORTS) "Maicon was not at the races at all in the first half at right-back. He was a passenger and it was like City were playing with 10 men. Cristiano Ronaldo kept coming inside him. "In the second-half, Vincent Kompany looked at what was happening and came across to that wing more. Ronaldo did not...

MANCHESTER UNITED VS CHELSEA #EPL TODAY AT OLD TRAFFORD STADIUM

MANCHESTER UNITED vs CHELSEA FC LEO #EPL USIKOSE NA USIKUBALI KUSIMULIWA #TheBattleAtOldTrafford:  Jioni ya leo miamba ya kabumbu la Uingereza inakutana katika mpambano unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua. Manchester United leo wanawakaribisha mahasimu wao Chelsea pale Old Trafford kwenye mchezo wa round ya pili ya Premier League. Ikumbukwe kuwa Katika mchezo wa kwanza walipokutana pale Stamford Bridge Chelsea waliwanyuka Man United 1-0,  goli lililofungwa na Alvaro Morata kwa kichwa. Kuna kama kauadui flani hivi kati ya makocha Antonio Conte wa Chelsea na José Mourinho wa Man United. Na huu ni uhasimu ambao kila mmoja wao anajaribu kuuficha na kuonesha kuwa hawana shida kati yao. Mourinho amenena kuwa game kati ya timu hizi mbili ni ya kawaida kwake kama game nyingine nyingine na hakuna chochote special kuihusu. Lukaku, Rashford, Martial,  Matic,  Pogba, De Gea  na wengineo wanategemewa kuongoza kikosi cha man United leo huku Morata, Fabregas, Pe...