Skip to main content

"JOSÉ MOURINHO NI BORA APIGE KIMYA TU"-SVEN-GORAN ERIKSSON

"José Mourinho ni bora apige kimya tu." - Sven-Goran Eriksson


Aliyewahi kuwa meneja wa kikosi cha taifa cha England Sven-Goran Eriksson anaamini kuwa meneja wa Manchester United, José Mourinho anakosea pale anapojibu shutuma au hukumu toka vyombo vya habari, na kwamba ingefaa abakie kimya. 


Msweden huyo siyo mgeni kwenye hukumu, shutuma za vyombo vya habari vya England kwa sababu aliwahi kukutana na adha kama hizo wakati alipokuwa kocha wa England kwa takribani miaka minne. 


José Mourinho amekutyana na adha kama hizo katika miaka yake ya ukocha kwenye premier league na inaonekana kwamba mambo yamekuwa mabaya zaidi baada ya Mourinho kuondoka kwenye kikao na wanahabari baada ya timu yake Man United kubugizwa bila huruma wala aibu kwa 3-0 wakiwa nyumbani Old Trafford mechi iliyopigwa usiku wa jumatatu iliyopita. 


"Siku zote mambo yako hivyo, unapokosolewa kama kocha ni bora ukae kimya" alisema Sven-Goran Eriksson akiliambia 'Sky Sport' 


"Usijaribu kujitetea kwa sababu matokeo yatakutetea, utajitetea kwa matokeo ya mchezo. Ukisoma kilichoandikwa gazetini, usijibu. 


Hasa pale unapoanza kubisha na wanahabari kamwe huwezi kuwashinda. Siku zote utapoteza tu kwa sababu wanahabari ndio waamuzi, wao ni waandishi. Hivyo kaa kimya, imamisha kichwa chako, endelea kuchapa kazi na waoneshe watu kuwa katika mechi ijayo itacheza mpira mzuri na utashinda." 


Lakini Mourinho haonekani kuchua ushauri kama huo wa Eriksson kwa sababu hasira zake zinaonekana kuzidi kichwa pale anapotokea kukosolewa hasa na wanahabari. 


#AbelRKayUpdates

Comments

Popular posts from this blog

MAKUNDI CHAMPIONS LEAGUE NA SHIRIKISHO AFRIKA

Yanga Sc kundi A Klabu Bingwa Afrika na Simba Sc kundi A Shirikisho Afrika. Hapo chini ndio mpangilio wa makundi na timu zake. Je, nani kati ya timu zetu za bongo atatoboa kwenda robo fainali? Weka maoni yako kwenye komenti tafadhali.

Hawa Ndiyo Real Madrid Waliowafunga Man City Champions League Jana Usiku

Man City wakiwa wanaongo za kwa 2-1 dhidi ya Real Madrid huku zikiwa zimebaki dakika si zaidi  ya tatu walionekana kama ingekuwa ni timu ya tatu ya Uingereza kuifunga Madrid kwenye uwanja wa Bernabeu. Lakini vijana hao wa Mancini badala ya kuinza kampeni yao kwa ushindi walijikuta wakiachwa nyuma na kuwaangalia Madrid wakiibuka na ushindi baada ya Karim Benzema kusawazisha na kisha Cristiano Ronaldo kufunga goli la tatu na la ushindi, goli lililomfanya bosi wao Jose Mourinho kuslide uwanjani akishangilia goli hilo na Ronaldo. This was the real happiness now from Ronaldo BBC football pundit Robbie Savage alikuwa uwanjani huku Bernabeu. (quoting from BBC SPORTS) "Maicon was not at the races at all in the first half at right-back. He was a passenger and it was like City were playing with 10 men. Cristiano Ronaldo kept coming inside him. "In the second-half, Vincent Kompany looked at what was happening and came across to that wing more. Ronaldo did not...

Cristiano Ronaldo Acheka, Lionel Messi Anuna!

Fifa World Cup 2018. Mechi za Kwanza. Ronaldo Acheka, Messi Anuna Tuziangalie mechi za ufunguzi, yaani mechi za kwanza kwa kika timu ama nchi kwenye mashindano ya fainali za kombe la dunia 2018 kule Urusi lakini hasa kwa mataifa mawili wanayotokea mastaa ama wapinzani wakubwa wawili ambao wanacheza kwenye La Liga kule Hispania, namaanisha Mreno  Cristiano Ronaldo na Muajentina Lionel Messi. Katika mechi yao Ureno ama Portugal vs Spain,  Ronaldo aliibuka shujaa baada ya yeye na wenzake kulazimishana droo ya 3-3 dhidi ya Hispania huku Ronaldo akiweka rekodi nyingine, akifunga hat trick yaani mabao matatu ndani ya mechi moja, kwa penati, shutu la mbali pamoja na free kick. Ronaldo akishangilia goli Kwa upande wa hasimu wake mkubwa Lionel Messi, yeye leo ameshindwa kabisa kufurukuta wakati taifa lake Argentina walipovaana na Iceland. Akipiga mashuti 11 hakufanikiwa kabisa kutikisa nyavu za Iceland kwani hata goli lao lilifungwa na Aguero. Huku akipata nafasi sawa na Ronaldo, yaani...