Skip to main content

UPENDO NI FARAJA

Simu yake iliita kwa sauti msikitini wakati wa swala, ilikuwa bahati mbaya.

Imama alitoa khutba fupi ya mawaidha baada ya swala akimwelezea jamaa huyo kama mfano wa waumini wazembe.

Waumini wengine walimlaumu baada ya swala kwa kuwasababishia usumbufu katika swala zao.

Mkewe naye hakubaki nyuma, wakati wakirudi nyumbani aliendelea kumpa maneno kuhusu uzembe wake mpaka wanaingia nyumbani.

Ndugu wengine walitikisa vichwa vyao kuonesha kukerwa sana na jambo alilolifanya.

Alionekana kufedheheka, kuaibika na kudhalilika sana. Hilo lilijionesha usoni mwake.

Hakukanyaga tena msikitini.

Jioni ile alielekea Baa.

Alionekana mwenye mhemko na kutetemeka.

Alimwaga kinywaji chake mezani, chupa ilidondoka kwa bahati mbaya na kuwamwagikia baadhi ya watu.

Wale waliomwagikiwa na kinywaji chake walimkimbilia. Alifumba macho akitrajia kuzabwa vibao au kuambiwa maneno makali.

Badala yake walimuuliza kama ameumizwa na kipande cha chupa iliyovunjika.

Mhudumu alimpa pole na kumpa tishu ajisafishe.

Mfanyakazi wa usafi alisafisha sakafu.

Meneji wa kike alimpa kinywaji kingine kufidia kinywaji chake. Pia alimkumbatia na kumpiga busu shavuni huku akimwambia: "Usihofu. Kila mtu hufanya makosa".

Tangu wakati huo hajaacha kwenda baa.

#FUNZO

Wakati mwingine tabia zetu kama waumini huwakimbiza watu wazuri na kuwasukumia motoni. Tunadhani kuwa tunajua kila kitu. Tunadhani kuwa tuna hakika mia kwa mia kuwa tutaingia Peponi.

Unaweza kubadilisha hali ya mambo kutokana na unavyoamiliana na watu, hasa pale wanapofanya makosa.

* Kama huwezi kuwa daraja la kuunganisha watu, basi usiwe ukuta wa kuwatenganisha. 

*Kama huwezi kuwa taa ya kuyaangazia mema ya watu, basi usiwe giza la kuzifunika juhudi zao.

* Kama huwezi kuwa maji yanayosaidia kustawisha mazao ya watu, basi usiwe mdudu anayeharibu mazao yao. 

* Kama huwezi kuwa chanjo ya uhai, basi usigeuke kuwa virusi vya kukatisha uhai.

* Kama huwezi kuwa penseli ya kuandikia furaha ya mtu, basi jaribu kuwa ufutio mzuri wa kuondosha huzuni yake. 

Daima tunaweza kuwa walinzi kwa wenzetu, tuwe na azma ya kuiponya dunia na kuifanya kuwa sehemu bora. Naam, tunaweza.

#UPENDO NI DARAJA KATI YAKO NA KILA KITU.

Imetafsiriwa na Maalim Ibrahim Kabuga.

#MoyoFoundation #Upendo #UislamuNiUpendo

Comments

Popular posts from this blog

These are Said to Be the Best Goalkeepers in the World, Ranking from 1-25

25. Stephane Ruffier, Saint-Etienne Had Stephane Ruffier not sustained a groin injury in 2011, Monaco might never have been relegated to Ligue 2. But he did, and they were, and that summer the then-24-year-old goalkeeper joined Saint-Etienne, rebuffing Manchester City in the progress. This season he played all 38 Ligue 1 matches for Les Verts for a second season in succession, conceding just 32 goals as his side finished a surprising fifth in the standings and qualified for the Europa League. 24. Pepe Reina, Liverpool Only Joe Hart kept more Premier League clean sheets than Pepe Reina in 2012-13. In a season that saw Liverpool finish a disappointing seventh in the English top-flight, the 30-year-old managed to keep things respectable from a defensive standpoint, conceding only 34 goals and stopping 88 per cent of the shots he faced. To finish the season he conceded just a single goal in his last four matches. 23. Mariano Andujar, Catania Only Parma managed ...

Hawa Ndiyo Real Madrid Waliowafunga Man City Champions League Jana Usiku

Man City wakiwa wanaongo za kwa 2-1 dhidi ya Real Madrid huku zikiwa zimebaki dakika si zaidi  ya tatu walionekana kama ingekuwa ni timu ya tatu ya Uingereza kuifunga Madrid kwenye uwanja wa Bernabeu. Lakini vijana hao wa Mancini badala ya kuinza kampeni yao kwa ushindi walijikuta wakiachwa nyuma na kuwaangalia Madrid wakiibuka na ushindi baada ya Karim Benzema kusawazisha na kisha Cristiano Ronaldo kufunga goli la tatu na la ushindi, goli lililomfanya bosi wao Jose Mourinho kuslide uwanjani akishangilia goli hilo na Ronaldo. This was the real happiness now from Ronaldo BBC football pundit Robbie Savage alikuwa uwanjani huku Bernabeu. (quoting from BBC SPORTS) "Maicon was not at the races at all in the first half at right-back. He was a passenger and it was like City were playing with 10 men. Cristiano Ronaldo kept coming inside him. "In the second-half, Vincent Kompany looked at what was happening and came across to that wing more. Ronaldo did not...

MANCHESTER UNITED VS CHELSEA #EPL TODAY AT OLD TRAFFORD STADIUM

MANCHESTER UNITED vs CHELSEA FC LEO #EPL USIKOSE NA USIKUBALI KUSIMULIWA #TheBattleAtOldTrafford:  Jioni ya leo miamba ya kabumbu la Uingereza inakutana katika mpambano unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua. Manchester United leo wanawakaribisha mahasimu wao Chelsea pale Old Trafford kwenye mchezo wa round ya pili ya Premier League. Ikumbukwe kuwa Katika mchezo wa kwanza walipokutana pale Stamford Bridge Chelsea waliwanyuka Man United 1-0,  goli lililofungwa na Alvaro Morata kwa kichwa. Kuna kama kauadui flani hivi kati ya makocha Antonio Conte wa Chelsea na José Mourinho wa Man United. Na huu ni uhasimu ambao kila mmoja wao anajaribu kuuficha na kuonesha kuwa hawana shida kati yao. Mourinho amenena kuwa game kati ya timu hizi mbili ni ya kawaida kwake kama game nyingine nyingine na hakuna chochote special kuihusu. Lukaku, Rashford, Martial,  Matic,  Pogba, De Gea  na wengineo wanategemewa kuongoza kikosi cha man United leo huku Morata, Fabregas, Pe...