Skip to main content

LILIVYOANDIKA GAZETI LA MWANANCHI KUHUSU "TUCTA" KUPINGA SHERIA YA PENSHENI

NIMELINUKUU GAZETI LA MWANANCHI "Limesheheni"

SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta) limeandaa maandamano ya amani kupinga mabadiliko ya  kupitishwa kwa sheria ya marekebisho ya mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA). Maandamano hayo yatafanyika Agosti 4 kuanzia viwanja vya Mnazi mmoja hadi katika Ofisi za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) iliyoko Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Tucta, Nicholus Mgaya alisema sheria ya mpya ya mifuko ya jamii inaeleza kuwa mfanyakazi mwanachama atakapotokea kuwa ameacha au ameachishwa kazi hawezi kuchukua mafao yake hadi atakapofikisha umri wa kustaafu ambao ni miaka 55 kwa hiari au miaka 60.

Katibu Mkuu wa Tucta, Nicholus Mgaya


Alisema kuwa mfanyakazi mwanachama wa mfuko wowote wa hifadhi ya jamii, akiacha au akiachishwa kazi akiwa na miaka 35 inabidi asubiri kwa miaka 20 alipwe mafao yake ya uzeeni. “Hiki ndio kipelngele cha sheria ambacho kimeleta taharuki kubwa miongoni mwa wafanyakazi wanachma wa mfuko hiyo,” alisema Mgaya.

Alisema wanatambua ukweli kuwa malipo ya uzeeni kwa mujibu wa dhana ya mifuko ya hifadhi ya jamii ni kwa ajili ya kumsaidia mwanachama aliyefikia umri wa uzeeni, hata hivyo walishabaini kuwa dhana hiyo ni vigumu kutekelezeka katika nchi yenye uchumi duni kama Tanzania.
Alisema sababu zinazosababisha ugumu huo ni kutokuwa na uhakika wa ajira, ajira kubwa hapa nchini kuwa mikononi mwa sekta binafsi, na pia mfumo wa hifadhi ya jamii kutokuwa na fao la watu wasiokuwa na ajira.

 Mgaya alisema kutokana na viwazo hivyo, hakuna utaratibu wa hifadhi kwa mwanachama aliyekosa ajira au anayetafuta katika kipindi ambacho ameachishwa kazi na kuhoji kwamba ataishije hadi kufikia miaka 55 kabla ya kupata ajira mahali pengine.

Alisema maisha ya watu hivi sasa yamezungukwa na mazingira hatarishi yenye magonjwa yasiyotibika, ajali nyingi, majanga ya moto mafuriko mambo ambayo yanachangia kwa kiasi kikubwa kupungua kwa umri wa kuishi.

Hata hivyo alisema wanataka kuona mabadiliko ya haraka yafanyike kwenye sheria hiyo ya hifadhi ya jamii ili fao la kujitoa liweze kurejeshwa au uandaliwe utaratibu muafaka utakaohakikisha mwanachama anarejeshewa michango yake na ya mwajiri pamoja na riba mara tu anapokoma uanachama wa mifuko hiyo.

Alisema Tucta haitasita kuchukua hatua za kisheria endapo mamlaka itaendelea kushikilia msimamo wake wa kubakiza kifungu hicho kinachomtaka mwanachama wa mfuko afikishe miaka 55 ndio alipwe mafao yake.

Aidha alisema Tucta wamesikitishwa na kushangazwa na kuwahi kutangazwa kwa mabadiliko ya sheria hiyo ya hifadhi ya jamii huku mchakato wake ukiwa bado haujakamilika baada ya kuridhiwa na Rais kama kupitia kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kutangaza kwenye gazeti la Serikali.

Mgaya alisema Tucta inataka mamlaka ya mdhibiti na msimamizi wa mfuko wa hifadhi ya jamii kuchukua jukumu la kutoa elimu kwa wanachama kuhusu sheria hiyo mpya kusaidia kupunguza malalamiko yasiyo ya lazima.

 Kwa upande wa Tucta Mkoa wa Dar es Salaam, Mratibu Musa Mwakalinga alisema wanapinga mabadiliko hayo kwani mishahara ya wafanyakazi walio wengi haiwatoshelezi hivyo watakosa mtaji wa kuanzisha ujasiriamali au kujiajiri wenyewe na kujikwamua baada ya ajira kukoma. Alisema mabadiliko hayo yataongeza umasikini kwa wafanyakazi pindi watakapoachishwa au kuacha kazi, wafanyakzi wengine watakaotaka wajiajiri wenyewe pindi ajira yao itakapositishwa.

 Alisema sheria hiyo inakusudia kutotoa huduma bora zitakazokidhi mahitaji mbalimbali ya msingi wa wafanyakazi ambao ni wanachama wa mifuko hiyo inayojali zaidi wafanyabiashara, ambao sio wenye mifuko kwa kuwajengea vitega uchumi ambavyo havimnufaishi mwanachama moja kwa moja.   


Comments

Popular posts from this blog

Britney Spears' Busy Vegas Weekend With New Beau. Via abc News

Britney Spears keeps it busy in Sin City. The "Scream & Shout" singer spent last weekend in Las Vegas but she wouldn't have come at all if her much-discussed Vegas residency was not a "done deal," the Las Vegas Sun reported. With new boyfriend David Lucado in tow, Spears flew to Vegas Friday and checked into Caesars Palace, the Sun reported. She attended a charity Cirque du Soleil performance, sneaking in just as the curtain went up and leaving just before the show ended. Spearstweeted a photo of herself, Lucado and her manager, Larry Rudolph, smiling in their seats together. Spears' management and production team met with executives at Caesars Entertainment Saturday, which owns Planet Hollywood, and then checked out the PH Live theater, where Brit will have her residency. Spears, Lucado and her entourage then lunched at the Meatball Spot restaurant, owned by Top Chef Seattle contestant Carla Pellegrino. The couple chowed down on meatball s...

Read What Shakira Says. Via Yahoo!

Looking at  Shakira  and her fabulous figure you might be surprised to learn it was only three months ago that she gave birth to son Milan. But the “Hips Don’t Lie” singer reveals that dropping the pounds was no cake walk. While promoting “The Voice” in Pasadena, California, on Monday, the blond bombshell revealed, "[Losing baby weight] is the only thing that’s been a little stressful … I knew I had to come back here to do ‘The Voice’ two months after I had delivered a baby. I didn’t have my four months of maternity like every woman on Earth has. I’m not trying to complain, but it’s been a process full of challenges.” Photo source: omg INSIDER & Yahoo The 36-year-old mama added that the pressure to shed the baby weight at record speed is something that she feels the previous generations didn't face. She said, “I think that our mothers and grandmothers weren’t under the pressure women of today are after delivering a baby. My dad says there’s nothing better than meat...

Jones With A Knee Surgery

Bleacher Report Writes: Manchester United defender Phil Jones is facing up to eight weeks on the sidelines after having surgery on a knee injury, the club has announced.   Jones, 20, has yet to make an appearance this season after hurting his back during pre-season and suffered this latest injury in training. "Phil Jones has had surgery on a knee meniscus tear sustained in training," said a United spokesman. "It will require six to eight weeks of rehabilitation." Jones, whose last competitive appearance for United was against Sunderland on the final day of last season, is understood to have suffered his latest injury in training earlier this week. The England international was sent for a scan on his right knee which has confirmed he requires an extensive period of rehabilitation. Jones was believed to be close to returning following back spasms when he damaged his knee. ...