Hatimaye bingwa mtetezi wa Kombe la Kagame Yanga ya Dar es Salaam leo imelitwaa kombe la kagame baada ya kumvurumisha Azam kwa magoli 2-0. Hamis Kiiza alifunga goli la kwanza la Yanga dakika chache kabla ya Half Time kabla ya Said Bahanuz kupachika bao la pili na kuwanyong'onyesha kabisa Azam katika dakika za majeruhi za kipindi cha pili. Nadi Haroub alimsifia kocha wake kwa kusema, "Siri kuu ni kocha wetu. Alitupa maelekezo mazuri nasi tukayafuata, ni kocha mzuri sana." Alisikika. Yanga imechukua kombe pamoja na dola 30,000 kama mshindi wa kwanza, huku Azam wakijinyakulia zawadi ya mshindi wa pili na kitita cha dola 20,000, wakati Vita Club ya Congo wakishika nafasi ya tatu baada ya kuwafunga APR magoli 2-1 na kunyakua donge la dola 10,000.
Brings You Global News!