Skip to main content

Posts

José Mourinho kuingiza pesa zaidi ya Messi kwenye kombe la dunia Juni 14

José Mourinho alamba dume dili la  Punditry kwenye kombe la dunia Russia Kocha wa Manchester United amepata dili kwa mara nyingine kama pundit wakati wa mashindano ya fainali za kombe la dunia yatakayofanyika nchini Russia kuanzia Juni 14 mwaka huu. José amepewa dili hiyo na kituo cha utangazaji cha Russia Today maarufu kama RT. Mou ataingiza kiasi cha pauni laki nne kwa siku kwa kazi hiyo ya uchambuzi atakayoifanya kwa kipindi hicho. Mzee huyu atanyakua mshiko mkubwa sana kwa kipindi chote hicho.

KUMBE N'GOLO KANTE ALIZIMIA MAZOEZINI SIKU 2 KABLA YA MECHI DHIDI YA MAN CITY

KUMBE N'GOLO KANTE ALIZIMIA MAZOEZINI SIKU 2 KABLA YA MECHI DHIDI YA MAN CITY Kiungo mahiri wa Chelsea Ng'olo kante alizimia kwenye mazoezi ya Chelsea Football Club na kuleta taharuki kubwa kwa wachezaji wenzake na kocha Antonio Conte.  Baadaye dokta wa timu alikuja Ssekunde chache baada ya tukio hilo. Lakini alipofanyiwa uchunguzi wa kina aligundulika yuko fit bila tatizo lolote la moyo. Pia inasemekana hali hiyo huwenda ilimtokea kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa ya baridi. Siku mechi ya na Man City alionekana kutokuwa fit tena na hivyo meneja wake kuamua kumpumzisha. Lakini anatarajiwa kurudi tena uwanjani siku ya Jumamosi wakati Chelsea watakapovaana na Crystal Palace.

KUMBE EDEN HAZARD ALICHEZESHWA NAMBA 9 YA UONGO😱😱😱

Kumbe Eden Hazard alichezeshwa namba 9 ya Uongo dhidi ya Man City!!!!! 😱😱😱 Eden Hazard wa Chelsea amelalamika na kulaumu mbinu iliyotumika katika mchezo wao dhidi ya Manchester City wa premier League ambapo timu yake walikula kichapo cha 1-0 pale Etihad Stadium jana Jumapili. Amedai kwamba kocha wake alimchezesha namba tisa ya uongo ili kuwazuga Man city na yeye mwenyewe hadi sasa hajui kwa nini ilikuwa hivyo.  Pia aliongeza kuwa haikuwa rahisi kwao kupambana dhidi ya vinara hao wa ligi kwani hawakuwa hata na uwezo wa kumiliki mpira ili waweze kufanya mashambulizi huku yeye mwenyewe akishuhudiwa kugusa mpira mara chache sana kitu ambacho sio kawaida kwake. Pia ilishuhudiwa Chelsea wakishindwa kabisa kupiga shuti hata moja lililolenga lango la wapinzani yaani shoot on target.

Chelsea wagawa Ubingwa kwa Man city. Wadorora uwanjani.

CHELSEA WAKABIDHI UBINGWA KWA MAN CITY Katika mchezo uliopigwa leo jioni tumeshuhudia Manchester City wakijichukulia pointi 3 kiulaini toka kwa Chelsea. Mchezo ulikuwa kama ni wa mazoezi kwa Man city ambao ni vinara wa ligi. Walimiliki mpira kwa asilimia kubwa sana na kuna wakati ilifikia hata man city 92% kwa Chelsea 18%. Kiukweli ni mechi ambayo haikuwa na ushindani kabisa.  HT:  0-0. Lakini kipindi cha pili ndio kilianza na goli lililofungwa na Fernando Silva. Goli lililodumu hadi mwisho wa mchezo.

FT: BRIGHTON Brighton & Hove Albion FC 2, Arsenal 1. JAHAZI LA ARSENAL LAZAMA TENA. MASKINI WENGER.... MASHABIKI WASEMA "WENGER OUT! "

Mzee Wenger amekula kichapo kingine leo toka kwa vijana wa Brighton Hove cha 2-1 katika mchezo wa premier League. Wiki iliyopita Arsenal walikutana na Manchester City Mara mbili kwenye EFL CUP na Premier League na kupewa kichapo cha 3-0 kwenye kila mechi. Baadhi ya mashabiki walionekana leo uwanjani wakinyanyua bango lililosomeka,  "Wenger out" Wakimaanisha kuwa wamechoshwa na vichapo mfululizo hivyo kocha hana budi kuondoka.

Diamond Platinumz kutumbuiza Ufunguzi wa Kombe la Dunia Juni 14

DIAMOND PLATINUMZ APEWA DILI NA FIFA WORLD CUP 2018 Msanii wa Bongo flava nchini Tanzania Dion Diamond Platinumz amekula dili ya ukweli toka Fifa ili aweze ku perform kwenye ufunguzi wa mashindano ya fainali za Kombe la Dunia yatakayofanyika nchini Russia kuanzia Juni 14 na kumalizika Julai 15. Diamond atashirikiana na  Jason Derulo wa Marekani pamoja na wanamuziki wengine maarufu wa Afrika.

Real Madrid 3, Getafe 1. CR7 akipiga mawili na kuweka rekodi ya magoli 300 kwa muda mfupi zaidi ya Lionel Messi

Real Madrid C.F. 3, Getafe C.F.1. Cristiano Ronaldo aweka rekodi. Huku CR7 akifikisha jumla ya magoli 300 ya La Liga akivunja rekodi ya Lionel Messi ambaye naye alishafikisha idadi hiyo hiyo ya magili lakini katika mechi 334 wakati C. Ronaldo ametumia mechi 286 kufikisha idadi hiyo ya magoli.