Skip to main content

Posts

Showing posts from December, 2015

LAST NIGHT.... SOUTHAMPTON vs ARSENAL... PALE UONGO UNAPOKUWA KWELI

Ni ngumu kuamini lakini ukweli siku zote unabaki kuwa ukweli kwa sababu kuu moja tu kwamba jambo limetokea na watu wamelishuhudia. Nilipokuwa nikisikiliza maneno toka kwa mashabiki wa Arsenal na matambo yao kwamba wanapanda kileleni kwa kuwa na uhakika kuwa wangemtwanga Southampton ilinifanya kuamini kwani niliona ni jambo linalowezekana sana. Lakini waswahili husema "mpira wadunda" wakimaanisha kwamba lolote laweza kutokea.... yaani ukweli waweza kuwa uongo na uongo kuwa ukweli. Sijui kwa nini nazunguka sana hivi.. ni kwamba mechi ya EPL ya late night yaani usiku mwingi ya jana matokeo yapo hivi na hayawezi futika wala mechi haiwezi kuahirishwa kwani kilichotokea ni halali. Southampton 4-0 Arsenal... Nimewajibika tu ku post.... Pia mechi nyingine iliiisha hivi. Newcastle 0-1 Everton .

MATOKEO YA EPL MECHI ZA LEO

STOKE CITY 2-0 MAN UNITED CHELSEA 2-2 WATFORD LIVERPOOL 1-0 LEICESTER MAN CITY 4-1 SUNDERLAND BORNMOUTH 0-0 CRYSTAL PALACE SPURS 3-0 NORWICH ASTON VILLA 1-1 WESTHAM UNITED WAKATI MECHI KATI YA SOUTHAMPTON VS ARSENAL ITAPIGWA BAADAE. MECHI INAYOENDELEA SASA NI NEWCASTLE VS EVERTON. HAKUNA TIMU ILIYOPATA GOLI HADI SASA .

Rais JPM Awa Gumzo Duniani..

Hivi sasa baadhi ya marais wa nchi mbalimbali wameanza kusifia jihudi, maarifa na kasi ya rais wa awamu ya tano ya Tanzania Dr. John Pombe Magufuli. JPM tangu aingie madarakani takribani mwezi mmoja amekuwa akifanya juhudi za dhati za kuikomboa nchi toka kwa mapapa ya ufusadi akianzia wizara ya fedha, bandari, TRA na sehemu nyingine akiwawajibisha wala rushwa, wakwepa kodi na wahujumu uchumi wa nchi huku wengine vibarua vyao vikiota nyasi na wengine hata kupelekwa mahakamani kujibu mashtaka. JPM alionekana leo ktk mtaa wa feri DSM akifanya usafi na majirani zake akitii amri aliyoitangaza mwenyewe ya kuwa maadhimisho ya uhuru wa Tanganyika ya 9 Disemba yasiwe na sherehe na badala yake siku hiyo iadhimishwe kwa kufanya usafi ili kutokomeza magonjwa yanayolitia taifa aibu hususan kipindupindu. Watanzania wengi kila mji wametii amri kwa furaha na kutoka tangu asubuhi wakifanya usafi. Wengi wameonekana kufurahia uamuzi wa mh JPM wa kutokuwa na sherehe za uhuru na kuifanya serikali kutunz

TANESCO DAR WATUMBUANA MAJIPU

Kama picha inavokuonesha hapo inaonekana TANESCO wamegundua mbinu za kuwajibishana kabla Rais Dr JPM hajawafikia. Vigogo saba ambao ni wahasibu wametumbuliwa na kutangazwa rasmi jana. Hongereni TANESCO ukanda wa Dar es salaam. Bado wale wa mikoani hasa Jiji la Arusha ambako kuna kero ya umeme isiyopimika .