Skip to main content

Posts

Showing posts from August, 2017

DAR: PAUL MAKONDA AZUIA AGIZO LA KUONDOA VIOO VYENYE TINT KWENYE MAGARI

HIVI PUNDE : PAUL MAKONDA AZUIA AGIZO LA KUONDOA TINT KWENYE MAGARI Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam, Paul Makonda amewaagiza Polisi jijini Dar kusitisha utekelezaji wa amri inayowataka wananchi wenye magari kuondoa tint kwenye vioo vya magari yao. Agizo hili ambalo hapo awali utekelezaji wake ilikuwa uanze kesho, Paul Makonda amesema litawaletea usumbufu wananchi kwani sababu za utekelezaji wake hazina mashiko. "Tafsiri yake ya kwanza ambayo agizo hilo inapeleka kwenye jamii ni kuwa wenye tinted kwenye vioo vya magari yao, kama sio wao basi wanaoyatumia, ni wahalifu. Jambo ambalo si kweli kwani yapo magari yanakuja yakiwa na vioo tinted, pia wengine wanaitumia tinted kama njia ya kujilinda dhidi ya watu wabaya hasa wakinamama," amesema Paul Makonda. "Aidha, mkoa wa Dar Es Salaam sio kisiwa, kuna watu wanaingia kila siku; Je, magari yao tu nataka wayapaki Chalinze?" ameuliza kwa mshangao Paul Makonda. Paul Makonda amehitimisha kwa kuwataka Polisi kutafuta njia sa

Raila Spent his Sunday with kids after ending up the campaigns. Read what he just said!

I had promised my granddaughters the day I get a day off the Campaign Trail it will be "their" day. That Sunday was today and they quickly came to collect! The pictures speak for themselves; we had a great time. I was surprised they let me on their equipment, I guess it's fair to say my early morning fitness training for Canaan is yielding results. The importance of family is immeasurable and I am thankful for the joys of it. Thanking all the people I interacted with today for the kindness they extended to my girls and I. Wishing you all a restful Sunday as we gear for the final lap into Canaan. Don't forget - 8-8-8 Niliahidi wajukuu wangu nikimaliza kampeni itakuwa siku yao. Hiyo siku Ikawa ni leo na wote walinikujia wakiwa pamoja. Picha zinadhihirisha ushahidi. Tulijivinjari. Nilishangazwa waliniruhusu kutumia vifaa vyao, nadhani mazoezi yangu ya asubuhi kuelekea Canaan yanazaa matunda. Umuhimu wa familia hauna kipimo na ninashukuru kwa furaha zake. Nashukuru wo

Arsenal Washinda Ngao ya Hisani (Community Shield) FT: Arsenal 1-1 Chelsea. Penalties: Arsenal 4-1 Chelsea. Na matukio mengi katika picha.

Hatimaye Mechi iliyokuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu ya Ngao ya Hisani kati ya Arsenal dhidi ya wenzao wa jiji la London Chelsea imepigwa na kukamilika kwa Arsenal kutwaa Ngao ya Hisani baada ya kuwabanjua mabingwa wa Epl 2016-2017 Chelsea kwa penati 4-1 baada ya kutoka sare ya 1-1 katika dakika 90. Katika mchezo huo uliokuwa safi,  wenye ushindani na uliotawaliwa na faulo za hapa na pale ulishuhudiwa mshambuliaji wa Chelsea Pedro akizawadiwa kadi nyekundu kwa mchezo mbaya na kuwafanya vinara Hao wa Epl kutoka jiji la London kumaliza mchezo huo wakiwa pungufu. Kadi za njano pia zilikuwa za kutosha kutokana na mchezo mbaya waliokuwa wakichezeana pande zote mbili.