Skip to main content

Posts

Showing posts from February, 2018

Manchester City 3, Arsenal 0. Man City new EFL Cup champions.

Magoli yaliyofungwa na Aguero,  Kompany na David Silva yaliwazamisha vijana wa Wenger, Arsenal na Kushindwa kabisa kufurukuta mbele ya miamba ya Pep Guardiola na kushuhudia man city wakitwaa Taji la EFL mbele yao katika dimba ya Wembley. Taji hilo linakuwa ni la kwanza tangu kwa Pep tangu awasili Etihad huku pia akifanya vizuri kwenye premier League na akitarajia kutwaa ubingwa huo.

#EPL. MANCHESTER UNITED 2, CHELSEA 1.

MANCHESTER UNITED 2, CHELSEA 1 Willian kwa Chelsea,  Lukaku na Lingard kwa Man United. Man of the match:  Romelu Lukaku,  one goal and one assist. #AbelRKayUpadates Vyombo vingi vya habari katika uchambuzi wao juu ya mechi hii viliipa Chelsea dalili kubwa ya kushinda game hii wakati vingine vikitoa uchambuzi wenye kuleta utata lakini ukifwatilia vilionesha kui favor the blues. Lakini nilipofwatilia mitandao ya kubeti ilionesha Manchester United kuizidi Chelsea kwa pointi kidogo, sasa sijui kama walikuwa wanajaribu kuwa deceive watu ili wapoteze bet zao. Hilo wanalijua wao. Nijualo mimi ni hili hapa: - FT:  Manchester United possession 44% na Chelsea 56%. Dak ya 32 willian anawaandikia Chelsea bao safi sana na kumfanya David De Gea kuchukia vile defenders wake waliacha gap kizembe na kusababisha kuwa nyuma kwa goli moja. Lakini dak 7 baadae yaani dak ya 39 zilipigwa pasi ndani ya 18 ya Chelsea na hadi kuwafanya watu wasahau kuwa hiyo ni man United. Pasi iliyomkuta Anthony Martial

MANCHESTER UNITED VS CHELSEA #EPL TODAY AT OLD TRAFFORD STADIUM

MANCHESTER UNITED vs CHELSEA FC LEO #EPL USIKOSE NA USIKUBALI KUSIMULIWA #TheBattleAtOldTrafford:  Jioni ya leo miamba ya kabumbu la Uingereza inakutana katika mpambano unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua. Manchester United leo wanawakaribisha mahasimu wao Chelsea pale Old Trafford kwenye mchezo wa round ya pili ya Premier League. Ikumbukwe kuwa Katika mchezo wa kwanza walipokutana pale Stamford Bridge Chelsea waliwanyuka Man United 1-0,  goli lililofungwa na Alvaro Morata kwa kichwa. Kuna kama kauadui flani hivi kati ya makocha Antonio Conte wa Chelsea na José Mourinho wa Man United. Na huu ni uhasimu ambao kila mmoja wao anajaribu kuuficha na kuonesha kuwa hawana shida kati yao. Mourinho amenena kuwa game kati ya timu hizi mbili ni ya kawaida kwake kama game nyingine nyingine na hakuna chochote special kuihusu. Lukaku, Rashford, Martial,  Matic,  Pogba, De Gea  na wengineo wanategemewa kuongoza kikosi cha man United leo huku Morata, Fabregas, Pedro, Alonso, Hazard, Moses, 

Angalia picha za Watford wakishangilia wakati wakiitafuna Chelsea kama nyama. FT: WATFORD 4-1 CHELSEA.

Arsenal wawazamisha Everton 5-1 bila huruma!

MANCHESTER UNITED WALIPA KISASI KWA HUDDERSFIELD. WASHINDA 2-0

Magoli yaliyofungwa na Romelu Lukaku na Alexis Sanchez yalitosha kuizamisha Huddersfield walipowatembelea Manchester United Old Trafford Jana Jumamosi katika mchezo uliochezwa saa 12 jioni kwa saa za Afrika Mashariki. Kichapo hicho walichotoa United ni kama kisasi kwani katika mzunguko wa kwanza walizimwa kwa 2-1 na Huddersfield. Japo mbali na kichapo ushindi huo umekuwa muhimu sana kwao kwani unawahakikishia kubaki nafasi ya pili na kupunguza umbali au utofauti wa alama kati yao na vinara wa ligi msimu huu Manchester City ambapo sasa kuna tofauti ya alama 13 kati yao.  Lukaku alifungua matumaini ya ushindi jana baada ya kuunganisha krosi safi iliyopigwa na Juan Mata kunako dakika ya 58 kipindi cha pili. Kunako dakika ya 68 Alexis Sanchez aliangushwa ndani ya 18 za Huddersfield na refa kuamuru ipigwe penati. Sanchez alipiga penati hiyo lakini kipa wa Huddersfield aliiona na kuicheza na kwa bahati mbaya kwake na nzuri kwa Sanchez ilimrudia na kuuweka mpira nyavuni na kuandika goli la