Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2018

Willian Kwenda Man United

Willian kwenda Man United Imefahamika kuwa tayari mazungumzo yameanza kati ya wawakilishi wa Man United na Willian kutoka Chelsea. Willian amekuwa katika kiwango bora sana katika miaka yake yote  5 akiwa na the blues lakini ikaanza kujitokeza tofauti kati yake na meneja wake Antonio Conte. Hali ilionekana kuwa mbaya zaidi pale Conte alipomwacha kwenye kikosi cha Chelsea kilichopambana na Man United kwenye fainali ya FA Cup. Meneja wa Man United yuko tayari kuhakikisha anapata saini ya Willian na kumuunganisha kwenye kikosi chake cha msimu wa 2018-2019.

Yaya Toure: Naweza kwenda Man United

Yaya Toure: Naweza kwenda Man United Pamoja na kuichezea Manchester City kwa takribani miaka nane, kiungo wa Man City, Yaya Toure amesema angeweza kufikiria kuhamia Manchester united iwapo nafasi hiyo itatokea. Toure anaondoka City baada ya kwisha  kwa msimu wa 2017-2018, na bado haijajulikana ataelekea wapi. "Ningependa kwenda mahali ambako  nitashinda na kupata mafanikio. Itakuwa vigumu kwangu siku moja kucheza dhidi ya City, lakini sina budi kufanya hivyo kwa ni sehemu ya maisha yangu. "Nimekuwa nikicheza mpira kwa muda mrefu, siwezi kufanya kazi za ofisini au kingine chochote, nijuacho Mimi ni mpira. "Kujiona katika club nyingine kwangu itakuwa ngumu. Nimekuwa sehemu ya City kwa muda mrefu. Nataka kusema kuwa nitaendelea kucheza kwenye level ya juu, Uefa au Ueropa league. "Nataka kucheza kwa miaka miwili zaidi. Lazima iwe  kwenye level ya juu halafu ndipo nifanye mambo mengine.

Breaking News: Huyu Ndiye Kocha Mpya Arsenal

FA CUP FINAL FT: CHELSEA 1-0 MANCHESTER UNITES

FA CUP FINAL FT: CHELSEA 1-0 MANCHESTER UNITED - Eden Hazard anatulia vizuri na kufunga penati dakika ya 22 baada ya kichezewa faulo na Phil Jones - Phil Jones anazawadiwa yellow card kwa kumchezea vibaga Hazard baada ya kuzidiwa mbio na kushindwa kumzuia - Chelsea wanatwaa ubingwa wa FA Cup 2017-2018 kwa kuwachapa Man United kwenye dimba la Wembley

FA CUP FINAL: MANCHESTER UNITED vs CHELSEA

FA CUP FINAL: MANCHESTER UNITED FC vs CHELSEA FC - Manchester United kukabiliana na Chelsea kwenye fainali za 137 za FA Cup leo Jumamosi usiku. - Timu zote mbili zikijaribu kujiokoa kwa kumaliza msimu angalao na kombe moja ukizingatia kutokuwa na msimu mzuri hasa kwa Chelsea ambao wameshindwa kupenya Top 4 wakimaliza ligi nafasi ya 5. - Kwa upande wa Jose Mourinho na Man United wanatazamia wanaonekana kuwa na nafasi nzuri zaidi ya kushinda FA Cup. - Yote kwa yote ni ama Mourinho au Conte kuibuka bingwa mpya wa FA cup. Wewe unaipa timu gani ushindi?

NEYMAR JR KWENDA MANCHESTER UNITED AU REAL MADRID MSIMU UJAO

Neymar Jr Kwenda Manchester United au Real Madrid Msimu Ujao Mshambuliaji wa PSG Neymar Jr amezungumzia mstakabali wake kwa msimu ujao na inawezekana akapata wakati mgumu kuchagua ka?a aende Manchester United ama Real Madrid. Neymar aliyehamia PSG akitokea Barcelona alishajutia kukurupuka kwake na kwenda Ufaransa ambako aliona soka la kule sio mahali pake na siyo kiwango chake akitaja kuwa halina ushindani wa kutosha. Manchester United na Real Madrid ndio timu ambazo zimeonesha nia kubwa ya kumtaka Neymar, huku kila mojawapo ikitaka kufanya hivyo kwa lengo la kuimarisha kikosi chake kwani imeonekana wazi wapinzani wao kwenye ligi zao wamejidhatiti vizuri mno. Manchester United wakimaliza ligi kwenye nafasi ya pili nyuma ya mabingwa wapya Mahasimu wao wa jadi Manchester City kwa tofauti ya pointi 19, na kwa upande wa Madrid wakishindwa kabisa kutamba mbele ya wapinzani wao wakuu Barcelona na kuwaacha wakitwaa ubingwa wa La Liga. Kwa mtazamo wako kama mpenzi wa soka, ungependa Neymar

ELIZABETH MICHAEL aka LULU SASA KUTUMIKIA KIFUNGO CHA NJE

Muigizaji Elizabeth Michael, maarufu Lulu,  amebadilishiwa adhabu na sasa anatumikia kifungo cha nje kwa amri ya Mahakama Kuu Tanzania. Magereza yathibitisha.

BARCELONA WAPOKEA KIPIGO CHA KIHISTORIA TOKA KWA LEVANTE. WAPIGWA 5-4 HUKU HAT-TRICK 2 ZIKIPIGWA

LEVANTE 5-4 BARCELONA: Game yenye hat-trick 2 - Magoli 9 yakitinga nyavuni huku ndoto ya wababe Barcelona kumaliza ligi bila kufungwa ikiyeyuka pamoja na Philippe Coutinho kuweka jitihada na kupiga hat-trick; Lakini Emmanuel Boateng nae akipiga matatu. - Philippe Coutinho hataisahau kamwe hat-trick yake ya kwanza kwa Barcelona. Alijitahidi zaidi ya wengine kuondoa aibu ya kihistoria akifunga magoli matatu lakini haikusaidia akijikuta yeye na timu yake wageuka jahazi lililozama. - Lionel Messi aliachwa apumzike na hiyo yaweza kuwa sababu rahisi kuwa kutokuwepo kwake kuliigharimu Barcelona.

MANCHESTER UNITED 1-0 WATFORD

Manchester United 1-0 Watford - Man United wamaliza msimu kww ushindi, Marcus Rashford akifunga goli pekee huku Michael.Carrick akiagwa rasmi ikiwa ni mechi yake ya mwisho. - Man United waliongoza kwa goli huku Michael Carrick na Juan Mata wakishirikiana na mpira kumfikia Marcus Rashford aliyeipatia United goli pekee. - Sergio Romero akiokoa mpira wa kichwa uliopigwa na Richarlson. - Mashabiki walipiga makofi wakiwa wamesimama wakiimba wimbo "stand up for Sir Alex Ferguson." - Michael Carrick akishangiliwa alipokuwa akitoka baada ya kucheza mechi yake ga mwisho kabla ya kustaafu.

NEWCASTLE 3-0 CHELSEA.

NEWCASTLE 3-0 CHELSEA. PICHA ZA KUTOSHA ZA MECHI HII. - Dwight Gayle na Ayoze Perez wanaipatia Newcastle ushindi mnono dhidi ya wanyonge Chelsea. - Matumaini ya Chelsea kumaliza top 4 yayeyuka aka Yaota mbawa aka imebaki ndoto. - Chelsea kushiriki Champions League kwa macho msimu ujao.