Skip to main content

UKWELI KUHUSU NGASSA KWENDA SIMBA HUU HAPA

 Picha mbilli za Alfan Mrisho Ngassa






Yule mshambuliaji wa Azam FC na Taifa Stars, Alfan Mrisho Ngassa amejiunga na timu ya Simba kwa donge la shilingi milioni 25, ukweli umethibitika.

Azam wamethibitisha hilo na kusema kuwa mchezaji huyo ameuzwa Simba na ataanza kuichezea timu hiyo kwenye msimu ujao wa ligi na kwamba sasa Simba wanayo haki ya kumuita mchezaji wao, alithibitisha Patrick Kahemele, Meneja wa Azam.

Hapo awali Azam walisema kuwa Simba walikua mstari a mbele kumuwania Ngassa aliyeenda Azam akitokea Yanga kwa kuvunja rekodi ya uhamisho Tanzania misimu miwili iliyopita.

Wakati wa michuano ya cecafa Kagame Cup, Azam walionesha nia ya kumuuza mchezaji huyo baada ya yeye kuonesha hadharani kutokuwa na mapenzi tena na timu hiyo kwa kuibusu nembo  ya timu ya Yanga.

Yanga pia walikuwa kwenye mbio za kumuwania mwana ndinga huyo lakini walitoa ofa ya shilingi milioni 20 tu na kukataa kuongeza dau, kitu ambacho kiliiweka Simba kwenye nafasi nzuri ya kumnyakuwa Ngassa.
Website ya Azam ilisema kwamba, "Tulipenda sana kumuuza Ngassa kwa Yanga lakini hawakutaka kutoa ofa nzuri."

Ngassa alijiunga na Azam mwaka 2010 kwa mshiko wa dola za marekani 40,000, pesa ambayo ilivunja rekodi za uhamisho kwa soka la Tanzania.

Alishawahi kwenda kufanya majaribio na timu ya Seatle Sounder FC na aliingia kama sub siku timu hiyo ilipokipiga na Man United kwenye mechi yao ya kirafiki.

Comments

Popular posts from this blog

MAKUNDI CHAMPIONS LEAGUE NA SHIRIKISHO AFRIKA

Yanga Sc kundi A Klabu Bingwa Afrika na Simba Sc kundi A Shirikisho Afrika. Hapo chini ndio mpangilio wa makundi na timu zake. Je, nani kati ya timu zetu za bongo atatoboa kwenda robo fainali? Weka maoni yako kwenye komenti tafadhali.

Hawa Ndiyo Real Madrid Waliowafunga Man City Champions League Jana Usiku

Man City wakiwa wanaongo za kwa 2-1 dhidi ya Real Madrid huku zikiwa zimebaki dakika si zaidi  ya tatu walionekana kama ingekuwa ni timu ya tatu ya Uingereza kuifunga Madrid kwenye uwanja wa Bernabeu. Lakini vijana hao wa Mancini badala ya kuinza kampeni yao kwa ushindi walijikuta wakiachwa nyuma na kuwaangalia Madrid wakiibuka na ushindi baada ya Karim Benzema kusawazisha na kisha Cristiano Ronaldo kufunga goli la tatu na la ushindi, goli lililomfanya bosi wao Jose Mourinho kuslide uwanjani akishangilia goli hilo na Ronaldo. This was the real happiness now from Ronaldo BBC football pundit Robbie Savage alikuwa uwanjani huku Bernabeu. (quoting from BBC SPORTS) "Maicon was not at the races at all in the first half at right-back. He was a passenger and it was like City were playing with 10 men. Cristiano Ronaldo kept coming inside him. "In the second-half, Vincent Kompany looked at what was happening and came across to that wing more. Ronaldo did not...

MANCHESTER UNITED VS CHELSEA #EPL TODAY AT OLD TRAFFORD STADIUM

MANCHESTER UNITED vs CHELSEA FC LEO #EPL USIKOSE NA USIKUBALI KUSIMULIWA #TheBattleAtOldTrafford:  Jioni ya leo miamba ya kabumbu la Uingereza inakutana katika mpambano unaotarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua. Manchester United leo wanawakaribisha mahasimu wao Chelsea pale Old Trafford kwenye mchezo wa round ya pili ya Premier League. Ikumbukwe kuwa Katika mchezo wa kwanza walipokutana pale Stamford Bridge Chelsea waliwanyuka Man United 1-0,  goli lililofungwa na Alvaro Morata kwa kichwa. Kuna kama kauadui flani hivi kati ya makocha Antonio Conte wa Chelsea na José Mourinho wa Man United. Na huu ni uhasimu ambao kila mmoja wao anajaribu kuuficha na kuonesha kuwa hawana shida kati yao. Mourinho amenena kuwa game kati ya timu hizi mbili ni ya kawaida kwake kama game nyingine nyingine na hakuna chochote special kuihusu. Lukaku, Rashford, Martial,  Matic,  Pogba, De Gea  na wengineo wanategemewa kuongoza kikosi cha man United leo huku Morata, Fabregas, Pe...