Skip to main content

WAGONJWA 37 WAPONA CORONA, 71 WASUBIRI VIPIMO VYA MWISHO

WAGONJWA 37 WAPONA CORONA, 71 WASUBIRI VIPIMO VYA MWISHO

Wagonjwa 37 waliokuwa wameambukizwa virusi vya Corona #COVID19 wamepona na kuruhusiwa kurejea nyumbani baada ya vipimo vya mwisho kuthibitisha kwamba hawana maambukizi.

“Watu hawa 108 hawana dalili zozote za ugonjwa kama vile homa au mwili kuchoka isipokuwa wapo katika vituo vya matibabu kusubiri vipimo vya mwisho ili kuthibika kwamba hawana virusi vya corona kabla ya kuruhusiwa kutoka vituoni,” amesema Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.

Waziri Ummy Mwalimu amewataka watu waliopona ugonjwa huo kuzingatia maelekezo ya wataalamu wa afya ili kujikinga na maambukizi mapya ya COVID-19 kwani zipo tafiti zilizofanyika nchi mbalimbali ikiwamo China zimeonyesha kuwa watu wanaweza kupata maambukizi mapya kama asilimia 14.

“Tunapenda kuwahimiza watu waliopona watoe elimu ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona (COVID-19) kwa jamii. Pia, Nitumie fursa hii kwa niaba ya Serikali kutoa shukrani zetu za thati kwa watumishi wa afya kwa kuendelea kutoa huduma kwa watu wenye maambukizi ya COVID-19. Asanteni sana watumishi wa afya,” amesema Waziri Ummy.

Waziri pia ametoa wito kwa watumishi wa afya kuendelea kutoa huduma za afya kwa watu wote wanaohitaji huduma za matibabu wakiwamo wenye dalili za ugonjwa wa Corona.

“Tumeona kumeanza tabia ambayo ni kinyume na taratibu za afya, hatutakiwi kuwakataa wagonjwa wenye dalili za maambukizi ya virusi vya Corona,” amesema Waziri Ummy.

Wakati huo Waziri Ummy Mwalimu ameishukuru kampuni ya Azam group kwa msaada wa sabuni 300 na fedha shilingi milioni 50 kwa ajili ya mapambano dhidi ya ugonjwa huo.

Msaada huo utatumika kwa chakula cha wagonjwa na usafi kwenye vituo vya tiba cha Temeke,Amana na Kisoka-Mloganzila

#AzamTv
#BongoOnlineNews

#Covid19 ni hatari. Jikinge. #Kinga ni bora kuliko #tiba


Comments

Thanh Mai said…
An toàn với con người và thân thiện môi trường: sàn gỗ công nghiệp chịu nước kronopolvietnam.com đều được kiểm duyệt chất lượng cẩn thận theo tiêu chuẩn chất lượng châu Âu, Độ thải formaldehyde cực thấp, theo tiêu thuẩn E1 (<0.05 ppm). không hề gây độc hại cho con người cũng như môi trường.

Popular posts from this blog

Joti naye auaga ukapera

Msanii wa maigizo ya vichekesho nchini maarufu kama Joti nae ameliaga kundi la makapera baada ya kufunga ndoa. Msanii Joti pia ni maarufu sana katika matangazo ya mtandao wa Tigo. Joti pia ni maarufu sana katika kuigiza sehemu mbalimbali kwani mara nyingi huigiza kama kijana wa kawaida, babu, mtoto na wakati mwingine huigiza kama msichana. Hongera sana Joti kwa kuoa! May your marriage last forever!

Ni Sawa Kwa Man City Kumuuza Mario Balotelli?

Ni mchezaji mwenye purukushani za kutosha awapo uwanjani. Purukushani zake ni za aina mbili. Zipo zile zinazoisaidia timu yake ya Man City pamoja na timu yake ya taifa ya Italy. Lakini pia zipo zile zinazowafanya siyo washabiki wa soka tu wakereke bali pia hata makocha wake. Lakini Balotelli ni mchezaji mwenye kipaji cha cha pekee kwa miongoni mwa wachezaji wa umri wake. Lakini sports director wa Man City, Brian Marwood, alikuwa na haya ya kusema kumuhusu Balotelli.   “I think that it’s important to make a good example. I think – and we all know who we are talking about – that you will get people within the system who do not show the right values and the right behavior. “In the main, we have a ­fantastic group of players here. I look at Pablo Zabaleta , I look at Vincent Kompany , I look at Joe Hart, Gareth Barry and Joleon Lescott. “I think we have a lot of players who can behave in the right way. You just have to make sure that they are the role models.” Katika ma